MWANAJESHI WA KUNDI LA KIISLAM HEZBOLLAH AELEZEA ALIVYOKUTANA NA MWANAUME YESU NA KUOKOKA SEHEMU YA II
Afshin Javid alikuwa ni askari wa Hezbollah ambaye aliyatoa maisha yake kikamilifu kwa ajili ya Allah. Katika maisha yake yote, alijifunza kumtii Allah na alikuwa tayari kufanya lolote, ikiwa ni pamoja na kufa kwa ajili ya Allah. Lakini baada ya kukutana uso kwa uso na Bwana Yesu, kila kitu kilibadilika. Sikiliza ushuhuda wake huu wenye nguvu sana, ambao si tu kwamba utakutoa machozi, kama yeye mwenyewe anavyoeleza kwa machozi mengi, bali pia utajua jinsi Bwana Yesu alivyo Mungu Mkuu na wa kweli ambaye, kila anayemtafuta kwa moyo wa kweli, anamwona. Hii ni sehemu ya pili ya ushuhuda wake. Ili kupata picha kamili, tafadhali anza kwa kusikiliza au kusoma ushuhuda wake, sehemu ya kwanza ******************* Nikasema, “Mbona sielewi? Jina lako ni nani?” Akasema, “Yesu Kristo.” Nikaanguka kifudifudi. Na nikalia! Na nikalia! Unajua, nikiwa kama Mwislamu, nilifundishwa kwamba mwanamume halii. Lakini nilishindwa kujizuia kwa sababu ...