Ubora wa mandhari wa Live Recording pamoja na Itifaki ya Mtiririko wa waimbaji ndio uliosahaulisha machungu ya Maelfu ya Wakazi wa Jiji la Dar-es-Salaam, Morogoro, Pwani , Zanzibar na nchi jirani Kenya waliochelewa kuingia ndani ya ukumbi wa CCC Upanga kufuatia utaratibu mpya wa usalama wakati wa kuingia kwenye Live Recording ya “Uko Hapa” ya Mwanamuziki John Lisu. Siku ya Jana katika Ukumbi wa CCC Upanga Mwanamuziki wa Injili John Leonard Lisu ameandika historia kwa mara nyingine kwa kurekodi albam ya pili ya DVD katika Ukumbi huo. Kabla ya John Lisu kupanda na Kuanza kurekodi watumishi wengine wa utangulizi walianza kazi ya kusafisha njia hiyo. Wanamuziki waliohudumu ni pamoja na Mbomby Johnson, Neema Gospel Kwaya, Pastor Paul Safari, Paul Clement na Abedinego Hango. John Lisu alipanda round ya kwanza na kurekodi nyimbo 12 mfululizo ambapo katika nyimbo hizo 12 amemshirikisha mwanamuziki maarufu wa Kenya Timothy Kaberia, pia amemshirikisha Mwanamuziki ...