Jumanne, 28 Februari 2012

MATUKIO KATIKA PICHA

Wiki iliyopita ilikuwa na matukio mengi, ikiwepo ibada ya J2, mkutano uliofanyika Penuel christian center kwa mchungaji Linde pamoja na maandalizi ya sikukuu ya WWK.



Praise Team wakiongoza Ibada Joshua, Vicent, Mrs Joshua na Faith.

Washirika wakipata maombezi kutoka kwa viongozi wa kanisa

Ev Kipwate akiongoza maombezi

Mch Mkongo akiombea wahitaji

Ev Kipwate akiombea wahitaji

Mpiga drum Papa John akihudumu

Baada ya ibada kulikuwa na maandalizi ya sikukuu ya wwk ambayo mwaka huu watasimamia mstari wa Isaya 61:1. katika maandalizi hayo wwk wameandaa chakula cha usiku kitaliwa tar 02/03/2012 kuanzia saa 12 jioni katika ukumbi wa kanisa wwk wamegawa kadi kwa washirika ili wawalete watu ambao bado hawajaokoka katika mlo huo ili wakutane na Muumba wao.


Kwaya ya WWK wakifanya mazoezi katika maandalizi ya sikukuu

Masololisti wa wwk

Mrs Malecela akisolo


Pia kama nilivyosema ilikuwa ni hitimisho la mkutano wa injiri uliofanyika katika tawi la Magomeni kule kigogo mkutano huo ulikuwa wa baraka sana watu wameokoka na kufunguliwa kutoka katika vifungo vya shetani, vilikuwepo vikundi mbali mbali vya uimbaji ikiwemo kwaya kongwe ya Magomeni Revival ambayo nayo ilihudumu mkutano huo baada ya kumaliza huduma kwa mch Thadeo, Mkutano huo ambao ulihudumiwa na wainjilisti 3 wa hapa hapa Dar ambao ni Ev Seiko wa Sinza, Ev , na mwinjilisti wa Taifa Ev Swila.  kwaya nyingine zilizohudumu ni Ebenezer Kutoka Tandale kwa Mch Mshama, kwaya ya Eagt kigogo, kwaya ya kanisa la tag Msasani na kulikuwa na waimbaji binafsi kama Kamanyonga, Mch Mshama (mrs) John shabani, kwa ujumla ulikuwa ni mkutano mzuri




Bloger Martin Malecela akiongoza kusifu  katika mkutano 

Kwaya EAGT Kigogo wakiimba

Mch Linde na Ev Kazimoto mc wa mkutano

Kwaya ya TAG Msasani wakiimba

Watu wakisifu

Mch Mwenyeji Linde akimkaribisha mhubiri

watoto wafuatilia mahubiri

Hata watu wazima nao walikuwepo

mama Mch Swila akisalimia makutano

Watumishi wa Mungu

Mtumishi akifuatilia mahubiri

Ev Kazimoto

Mzima na John wakati wa sifa

Mch kutoka Tabora anayechunga kati ya makanisa 3 aliyofungua Mch Kabanda

Mch Mshama wa Tandale TAG alikuwepo

Mch Mwenyeji Linde

Mzee Ndauka na washirika wengine wakisikiliza mahubiri

Mwinj Swila

Wahudumu wakikemea pepo

Mwinj Swila akiongoza watu sala ya toba

Ev Kazomoto akiombea watu

washirika wakifuatilia mahubiri
Mathayo 6:33 Utafuteni kwanza ufalme wake na haki yake na hayo mengine mtazidishiwa.

Jumatatu, 20 Februari 2012

Ufunguzi wa kanisa la Mch Thadeo (Midizini Healing Center)

Tawi jipya la kanisa la TAG Magomeni limefunguliwa jana Tar 19/02/2012 ambalo litaongozwa na Mch Thadeo, kabla ya ufunguzi huo ulifanyika mkutano wa ndani wa injili ambao uliandaliwa na kanisa la TAG Magomeni ambapo mwinjilisti chipukizi Ev Nelson Kazimoto alihubiri siku zote za mkutano na usiku kulikuwa na cinema ya Yesu ilikuwa inaonyeshwa ambayo nayo ilikusanya watu wengi, katika mkutano huo Mungu alionekana kwa kuponya na kufungua waliofungwa na watu waliokoka, ufunguzi wa kanisa hilo unafanya kanisa la Magomeni kuwa na matawi yasiyopunguwa 6 ambayo ni Mch Steven, Mch C Lijongwa, Mch Kabanda ambaye yeye ana makanisa mawili wote hawa wako Tabora na  Mch J. Linde kigogo, Mch Mshama Tandale, na Mch Thadeo ambaye ameanzisha Midizini. na bado mpango wa kanisa ni kufungua matawi zaidi na kuwapeleka watu katika vyuo ya Biblia na chuo cha kupanda makanisa ili kutimiza mpango mkakati wa TAG Taifa wa miaka 10 ya mavuno. niliongea na Mwenyekiti wa kamati ya uinjilisti ambae alisema mwaka huu wanategemea kufanya mkutano mkubwa Tabora kwa Mch Kabanda mwezi wa 6 na mikutano mingine katika matawi ya kanisa.

zifuatazo ni baadhi ya picha za matukio hayo


Washirika wa midizini wakiwa katika ibada ya kusifu na kuabudu jpili ya kwanza ya ufunguzi wa kanisa.

Mch kiongozi wa Midizini healing center ndg  Thadeo akihubiri katika ibada ya ufunguzi.

Wanakwaya wa Revival kutoka TAG Magomeni wakiongoza kipindi cha kusifu na kuabudu na ilihudumu na kwenye mkutano uliofanyika hapo Midizini

Kipindi cha sifa.
Mathayo 6:33 Utafuteni kwanza ufalme wake na haki yake na hayo mengine mtazidishiwa.

Ijumaa, 17 Februari 2012

Rose Mhando Apata Mkataba Mnono, awapita hata akina AY, FA, NK


Hivi karibuni kampuni ya kusambaza kazi za waimbaji duniani ya Sony imeingia mkataba na muimbaji wa nyimbo za Injili rose mhando kwa muda wa miaka mitano. kampuni hiyo ambayo makao yake ni Africa kusini ilimtangaza Rose mbele za wadau mbalimbali wa mziki wakiwapo wanahabari wanamziki ya bongo fleva, waandaaji wa mziki na wadau wengine katika hotel ya kitali ya kilimanjaro. kuchaguliwa kwake kulitanguliwa na mchakato wa kutafuta waimbaji ambapo kati ya watu zaidi ya 130 hivi walifanyiwa mchujo na kupatikana mtu mmoja mchakato huo ulihusisha na matoleo ya kazi zake ambazo alisha toa na mauzo aliyofanyika katika kazi zake za zamani ambapo kuna toleo ambalo aliwahi kuuza copi 5,000,000. hiyo mkataba alioingia utamfanya azunguke nchi nyingi zaidi ndani ya Afrika na nje ya Afrika kufanya huduma hiyo ya uimbaji. tarifa za wandishi wengi zimesema kuwa huu ni mkataba wa kwanza waimbaji wa nyimbo za injili kufanywa na kampuni kubwaa ya kimataifa ya Sony hapa nchini, lakini huko nyuma mwimbaji mwingine wa nyimbo za injili Pendo Kilahilo naye alisha wahi kuingia mkataba na kampuni hiyo ya Sony alipokuwa Sauth Africa na kubadilisha baadhi ya nyimbo zake na kuimbwa katika Lugha nyingine zaidi ya kiswahili kuwa za kimataifa zaidi ili kupata soko zaidi. kupata kwa nafasi hii kwa Rose inaleta changamoto katika tasnia ya nyimbo za injili na kufanya watu wajue kuwa kuimba ni kazi kama kazi nyingine ambazo kama mtu atakuwa siliasi basi atatoka kimaisha


Rose Mhando akiwa amekumbatiana na Bahati Bukuku baada ya kutangwa na kuingia mkataba mnono na Kampuni ya Mziki ya Sony.

Rose ambaye anatamba na albamu yake ya utamu wa Yesu amekuwa akifanya vizuri na kusababisha mziki wa injili kuwa na soko hapa nchini tofauti na mziki mingine hata kuwafanya wana mziki wa kidunia kuvutiwa na hata wengine kurekodi nyimbo za injili kama alivyofanya Mr Nice ambapo mwishoni mwa mwaka jana alitoa albam yake ya nyimbo za injili na huku yeye ni mwimbaji wa dunia na hata baadhi ya wanamziki wa kidunia nilioongea nao wanasema siku hizi nyimbo za ijili zinapigwa sana kwenye sherehe kuliko nyimbo zozote ha kwenye sherehe za kislam na waslamu wengi nao ni wadau wazuri wa nyimbo hizo wengi wananunua cd na hata kuweka nyimbo hizo kwenye simu zao. vilevile Rose aliwahi kuwika kwenye albamu zake za zamani na ile kiatu kivue aliyoshirikishwa. aidha albamu yake ya jipange sawasawa inaongoza kwa kuuzwa katika albamu zake kwa zaidi ya copi 5000,000. albam yake 1 tu ndiyo haikufanya vizuri katika soko nayo ni zawadi ya krismas ambayo ilikuwa ya pili kutoa baada ile ya kwanza, vile vile Rose amewahi kuwika katika albam aliyolekodi na kwaya ya cimuli Anglican Dodoma na kuna single kadha ambazo amerekodi katika haleluya collection.
Madam Lita akiongea jambo kwenye mkutano huo na nyuma anaonekana mtayarishaji wa mziki wa bongo fleva ambaye haamili kilichotokea

Rose akiwa kwenye picha ya pamoja na baadhi ya wanamziki maaruufu wa bongo fleva kutoka kulia ni mwana FA, AY, Daimond, Rose, Bahati Bukuku, Mwl John Shabani.

ninamuombea Rose ili aweze kuwakilisha vilivyo katika mkataba huo alioupata ambao naamini umefungua ukrasa mpya kuonyesha hata nyimbo za injili bado zinaweza kuwa juu hata kufanya makampuni ya nje ya nchi kuona unafaa kusambazwa duniani ukiachilia mbali hizi kampuni za hapa kwetu ambazo huishia hapa nchini tu na bado hawana uwezo wa kutosha kutangaza kazi za waimbaji kimataifa. Mungu mbariki Rose \Mungu wabariki waimbaji wa injili wa Tanzania.
Mathayo 6:33 Utafuteni kwanza ufalme wake na haki yake na hayo mengine mtazidishiwa.

Alhamisi, 2 Februari 2012

Jua history ya mwimbaji maarufu wa gospel Ron Kenoly



 Dr Ron Kenoly
"God is the same yesterday, today and forever. But we're not. We change with time." Those are the words of a man who knows a great deal about change, transition and life in the Lord. From the time Dr. Ron Kenoly was born on December 6, 1944, until now, a great deal has transpired. Both the man and his ministry have evolved. At 65, he has gone from being a military man to a Rhythm and Blues artist, then from a Sunday morning congregational hymn leader to the most popular Praise and Worship leader in the country. "God created the world so we would go through seasons. Each season brings about a change." Dr. Kenoly's life is one that has gone through many seasons, all designed by God to bring him to a place of serving the Lord and leading millions of people into His presence.


After graduating from High School in his birthplace, Coffeyville, Kansas, Kenoly ventured out to Hollywood, California. When plans to make it in the big city fell through, he joined the Air Force in 1965. It was in the military that he met and married Tavita, his wife of 42 years. It was also there that the humble beginnings of his music career were launched. Kenoly joined the Mellow Fellows, a top 40 cover band that toured military bases. In 1968, he left the Air Force and the Mellows Fellows behind and shipped out to the City of Angels to go after his passion- music.



"As a child I remember seeing Sammy Davis Jr. and Nat King Cole for the first time. I was so impressed as I watched two Black men grace a national stage. I knew right then that was what I wanted." So for the next few years, Kenoly poured all of his energy into making his childhood dream a reality. He sang demos of Jimmy Web songs, like the 70's hit "Up, Up and Away," for the Audio Arts label. The label also released Kenoly's first single, "The Glory of Your Love (Mine Eyes Have Seen)." Success in the R&B arena came after he signed with A&M Records. Under that label, he cranked out hits like, "Soul Vaccination."

All the success was taxing on Kenoly's family. His marriage suffered, he neglected his kids and soon the home was close to ruin. But then God stepped in. "My wife rededicated her life to the Lord in 1975 and began praying for our family's healing. I could see the changes in her life and that's when the

lights came on for me." Again, Kenoly had to enter into another transitional season of his life. The family stayed in LA for another year as he fulfilled R&B contractual agreements. Then they moved out to Oakland, CA. While working in a service industry position, Kenoly allowed the Lord to work on him, teaching him how to be a husband and father. While teaching music and physical education at Alameda College from 1978 to 1982, Kenoly tried unsuccessfully to get a gospel record deal. "Then one night I sat alone in church for hours playing, singing, praying and worshipping the Lord. I found the heart of God through worship. From then on, the record companies ceased to matter. The Lord met me and showed me so much that I felt I had gone beyond what any company could offer me."

So in 1983, Kenoly produced his custom-made album, "You Ought to Listen to This." He sold the album wherever he sang. Soon, offers to lead praise and worship came flooding in from churches in the area. In 1985, Pastor Dick Bernal who founded the Jubilee Christian Center in San Jose, CA, invited Kenoly to be the church's Minister of Music. Shortly after, Don Moen of Integrity Music heard about Kenoly's music. In 1991, Integrity released Kenoly's first gospel album, "Jesus is Alive." "Lift Him Up," "God is Able," "Sing Out," "Welcome Home," "High Places," "Majesty" and "We Offer Praises" all followed Kenoly's first surprise hit.

With all 8 albums, Kenoly sold more than 4 million copies. Two albums received gold record sale status and 3 live videos went gold. Kenoly received 19 GMA Dove Award nominations and won 1 Dove Award for "Welcome Home." "Every season of my life has had its own lessons. I think that's true for all of us. You never learn persistence until you have something you really want. You never learn faith until you have trials to test who you are and what you believe." Having learned and been tested, now with 8 successful records under his belt, Kenoly again knew it was time for change. In 1999 he felt the call to move from California out to the East Coast. Again, he picked up his family and moved them and his ministry out to Orlando, FL. It was after that move that he instituted new programs and endeavors. The Lord purposed in his heart to start the Academy of Praise, a mentoring program for Praise and Worship leaders and those in Christian music. The first conference was held at Kenoly's home church, Faith World Center, and more than 1000 people attended. Kenoly's goal is to take the Academy to different countries and regions of the world.

The new experiences in Kenoly's life even influenced his music. "As beats change, as technology changes, as the approach changes, I will change with them. I won't be like the people in the Bible who stayed in the wilderness and died because they weren't willing to crossover." So following the trend of progression in the music industry, Kenoly tried something different with his 9th album, "Dwell in the House." This is the only CD not recorded live. The studio album, released in 2001, has more radio and popular appeal than his previous projects. Kenoly calls it Praise and Worship with a new Millennium edge.

It's been quite a journey for the man who God has used to sow into the lives of millions across the globe. He's had to change and adjust along the way. But he says his purpose and his message have remained the same. "God desires His people to be in His presence. It's what He's been saying since the beginning of time. What I do is just a 21st century approach to getting God's people back to His presence through worship. For the remainder of my life, I plan to put myself in a position to lead others in worship and praise, and to help those that I lead realize a higher level in their praise and worship experience." "I will bless the Lord at all times and His praise will continually be in my mouth."


Dr Ron and his wife


Mathayo 6:33 Utafuteni kwanza ufalme wake na haki yake na hayo mengine mtazidishiwa.

Ron Kenoly & Don Moen Above All Our Heart



Mathayo 6:33 Utafuteni kwanza ufalme wake na haki yake na hayo mengine mtazidishiwa.

Jumatano, 1 Februari 2012

FAHAMU NINI MAANA KUSIFU NA KUABUDU KATIKA BIBLIA

Nini maana ya kusifu na kuabudu


KUSIFU NA KUABUDU ni maneno tofauti na yana maana tofauti
1. kusifu

MAANA --- nikuelezea wasifu au wajihi za kitu au mtu. Sasa tunaposema tunamsifu Mungu inamaanisha ni KWA KUMUINUA JUU, KUSHUKURU KUMPAZIA SAUTI,KUFANYIA SWANGWE, KUJISHUSHA CHINI YAKE KWA UNYEYEKEVU,nk Zaburi 100:4

Neno hili kusifu kwa kiebrania lilikuwa na maana ya;
Tehila, yaani kutamka neno kwa kuongeza vionjo na mbwembwe zaidi. Mfano neno haleluya unalitamka (Ha, ha leluya huuu eee) Tehila ni kuwa kama kichaa unaposifu au kuabudu kwa utukufu wa Bwana. (Nilidhani labda hapa ndipo waswahili walipopata neno taahila).

Yadaa yaani kujiachia kwa Mungu (you just surrender yourself to the Lord).
Barak yaani kusaluti mbele za Bwana. Ni kuonyesha kwamba ni yeye peke yake anayestahili heshima na utukufu. Huwezi kumpigia saluti mtu usiyemwona, hivyo ni kwa njia ya kumwabudu Mungu katika roho na kweli ndipo tunapomwona kama alivyo na utukufu wake

2. Kuabudu
Neno la Kiebrania shachah lina maana ya kuabudu, kusujudia, kuinama kwa kuonesha unyenyekevu, kuonesha heshima kubwa au kuanguka kifudifudi. Neno la Agano la Kale proskuneo halikadhalika lina maana ya kubusu mkono, au kupiga magoti na kugusa ardhi kwa paji la uso kwa unyenyekevu mkuu. Maneno mengine mawili ya kuabudu yana maana ya kutumika, kufanya ibada Takatifu na kumtolea Mungu Sadaka.

Waache Watu Wangu Waondoke, Ili Wapate Kunitumikia, Dai hili Mungu alilolirudia mara kwa mara lilipelekea Farao kuwaruhusu watu wa Mungu kutoka Misri. Tangu wakati huo, Mungu, Mungu mwenye wivu, amekuwa akipambana na watu wake akiwazuilia kuabudu miungu mingine na sanamu, na badala yake wamwabudu Mungu aliye hai na wa kweli. Kutoka 7:16
Ibada ni kumtukuza Mungu na kumfurahia daima. Mungu anawatafuta watu wa kumwabudu, na kufanya ibada ndiyo wito wetu wa kwanza (Yn4:23 Lakini saa yaja, tena ipo, ambapo wale waabuduo halisi, watamwabudu Baba katika roho na kweli. Watu wanaoabudu namna hii, ndio Baba anawatafuta. Msitari wa 24 unasema Mungu ni Roho na wote wanaomwabudu imewapasa kumwabudu katika roho na kweli.). Ibada ya kweli ni pale tunapomruhusu Roho Mtakatifu atuongoze kutoka katika roho zetu au mioyo yetu kuabudu katika roho na katika kweli na sio tumaini letu ktk miiliau akili zetu Flp 3:3.

Ibada ni tendo la thamani kubwa, ni la kipekee na linamhusu Mungu (utatu mtakatifu) ambao peke yao wanastahili. Lucifer, aliyekuwa mhusika mkuu wa ibada huko mbinguni, alitaka ibada hiyo iwe kwa ajili yake, maana yake aabudiwe yeye badala ya Mungu; na hilo ndilo lililopelekea kuanguka kwake (Isaya 14 na Ezekieli 28). Hata wakati fulani alitaka Yesu amsujudie ili eti ampe falme zote za dunia lakini Bwana alikataa Mt4:8-10.

Kwa hiyo kuabudu ni ibada na tunaposema ibada sio zile taratibu za kibinadamu tulizojipangia katika ibada zetu za siku za leo, ibada za leo tumeweka mambo mengi sana na yanatumia muda mwingi sana kuliko ile maana hasa ambayo mungu aliikusudia katika agano la kale utana ibada zilikuwa zinafaywa kwa mambo makuu 2 neno la Mungu, na Kuabudu.

Kuabudu ni sehemu ya maisha wanadamu tumeumbiwa kuabudu, watuwezi kuishi bila kuabudu hapa haijalishi unaabudu nini!!! Unaweza kuwa unaabudu Mungu wa kweli au miungu kama ambavyo ukisoma bilia utaona kuna miungu mingi inatajwa mfano Baali, Dagon ink na hata leo iko miungu mingi ambayo wanadamu wanaiabudu lakini wa kuabudiwa ni mmoja tu. Na katika biblia tunaona kuaudu kwa mara ya kwanza kulikofanywa na Ibrahimu kutoka katika kitabu cha mwanzo 12: 8 Psalms 34:1 inaonyesha tunatakiwa kumwabudu Mungu kila wakati.

Kwanini tuabudu
kuabudu ni agizo kutoka kwa Mungu kutoka 20 2-4 . Psalm 96:9, Psalm 29:2 Tunapomwabudu mungu naye Mungu hufurahiwa na sisi Zephaniah 3:17 Rom 12:1-2

Your Worship = Your View of God
jinsi unavyoabudu ndiyo mwonekano wa mungu ulivyo ndani yako, haijarishi unaabudu wapi uwe peke yako au mko wengi kama unaabudu kwa kutokumaanisha au kumaanisha itajulikana tu na hivyo ndivyo mtu anaweza kujua ni jinsi gani mtazamo wako kwa Mungu wako.

KUNA NGUVU KATIKA KUSIFU NA KUABUDU
Yoshua 6:20 Matendo 16:23-26 zinaonyesha ambavyo kwa kutumia kusifu tu Mungu alishuka na kufanya lile lililokuwa hitaji lao.

Kusifu kunamfukuza adui
Psalms 50:23. 2 Nyak 20:22. Ukiwa unasifu na kuabudu humfukuza adui mbali kutokana na ukiwa kwenye ibada Mungu hushuka maana yeye anasema anakaa katikati ya sifa hivyo palipo na Mungu shetani hawezi kuwepo lazima akae mbali.akimbie mbali kabisa maana kunakuwepo na uwepo wa bwana wa Majeshi.

Je, ni wakati gani tuabudu?
Ni niyakati zote zinafaa kumwabudu Mungu. Kwa nyakati zilizotengwa Zaburi ya 100 inatuelekeza namna ya kuanza, lakini zaidi ya yote tunapaswa kuishi maisha ya ibada bila kukoma. Kwa kila tunapopumua, kwa kila wazo, kwa neno na tendo, tunapaswa kumwabudu Mungu wetu mzuri tunayemtumikia milele na milele Zab 145:1,2

mwa 12:6- Siku zilipita na watu wakafanyia ibada kwenye Hekalu na kwenye masinagogi; lakini siku hizi miili yetu ni hekalu la Mungu 1Kor 6:19 tu hekalu la Mungu sisi ibada zinatakiwa zifanyike kila wakati na si mara moja kwa wiki kama wengine wanavyo dhani.

Je, Tunafanyaje Ibada?
Biblia inatufahamisha jinsi watu walivyotumia mioyo yao, mawazo yao, mikono yao, viganja vyao, miguu yao, na midomo yao katika uimbaji. Walipaza sauti zao kwa furaha na kusujudu, kucheza, kusifu, kubariki na kushukuru.

Maneno kama halal na haleluya kutoka katika Zaburi yana maana ya kusifu, kumwinua na kumwadhimisha Bwana. Neno Yadah lina maana ya kunyoosha mikono hewani, na neno barak lina maana ya kupiga magoti katika ibada ya kumbariki Mungu. Kuitoa miili yetu katika kumhudumia Mungu na mwanadamu ni ibada pia (Rum 12:1). Watu pia humwabudu Mungu katika sanaa zao, katika uandishi wao, katika michezo ya kuigiza, katika muziki, katika usanifu wa majengo, na hata katika utoaji wa fedha zao kwa ajili ya Injili.

Kusifu na kuabudu sio kuimba tu
Watu wengi wanajua kuwa kusifu na kuabudu ni kuimba tu hapana kuna njia nyingi za kusifu au kuabudu, unaweza kutumia sanaa nyingine kumwabudu mungu au watu wengine wakamwabudu Mungu mf maigizo, ngonjera, shaili, uchoraji, upambaji au unakshi wa vitu, kujenga .nk

Ibada Kanisani
KatIka kanisa makusanyiko yetu yanapaswa kujawa na zaburi, nyimbo, na tenzi za rohoni ambazo zinaweza kuongozwa na Roho katika lugha mpya anazotupatia Yeye. Kwahiyo mikutano mingi ya kisasa haina tofauti sana na burudani za kikristo kama kwenye kumbi za starehe. Watu huwa wanaangalia tu, lakini je, wanaabudu? Uwepo wa Mungu na Roho wake katika ibada zetu utawafanya watu wasioamini kuanguka chini na kuabudu (Kol 3:16) (1Kor 14:15,16,25,26) (Efe 5:19) (Mdo 2:4).

Ibada Ya Kweli Ina Gharama
Biblia inazungumzia habari za sadaka za kusifu. Daudi alicheza mbele za Bwana kwa nguvu zake zote, na akakataa kumtolea Mungu kafara ambayo isingemgharimu cho chote (2Sam 6:14; 24:24). Wale mamajusi wa Mashariki walitoa zawadi za gharama kubwa walipokuja kumwabudu Yesu (Mt 2:9-12), na mwanamke mmoja alimpaka Yesu kwa mafuta ya gharama kubwa, akamwosha miguu yake kwa machozi yake, na kuifuta kwa nywele zake (Lk 7:36-50). Hivyo ibada yoyote inaambatana na kutoa tena vitu vyetu vya thamani.

Tunapaswa kumsifu Mungu kwa jinsi alivyo na kwa matendo yake; lakini Mungu mwenyewe anawatafuta na anawataka wafanya ibada, na si mradi ibada tu. Kusifu kwaweza kufanywa hadharani, lakini ibada mara zote ni jambo la ndani ya moyo. Kusifu mara zote kunaweza kuonekana au kusikika, lakini kuabudu yaweza kuwa ya kimyakimya na iliyofichika. Kusifu kunaonekana, kuna kutumia nguvu, kuna misisimko na furaha; lakini ibada mara zote ni heshima na hofu katika uwepo wa Mungu.
Biblia pekee inatuonesha jinsi Mungu anavyo hitaji na kutamani kuabudiwa na yeye pekee yake ndiyo anayestahili kuabudiwa.

Kusifu na kuabudu kwa siku za leo
Katika siku za leo kuna ufinyu wa mafundisho katika kusifu na kuabudu na ndiyo maana ya kuanda somo hili ili tupanuane mawazo. Watu wengi wa leo wanadhani kusifu ni kuimba kwa nyimbo zenye midundo ya harakaharaka(zouk&sebene) na ukipunguza spidi ndo kuabudu. Hasha tunaposema kusifu inatokana na maneno yaliyopon kwenye wimbo husika kweli ni ya kusifu, kama ni maneno ya kusifu tunasema ni wimbo wa sifa haijarishi speed inayotumika na hali kadhalika nyimbo za kuabudu. Watu katika kipengele hiki huwa wanachakanya nyimbo utakuta wakati wa kusifu anaimba wimbo wa kutia moyo au wa maombi, kinachotakiwa ni kujua kuwa kila jambo lina wakati wake ziiko nyimbo za mazishi, kufariji, kutia moyo, za maombi, za kusifu , na za kuabudu nk sasa usichanganye kwenye kusifu wewe unaimba parapanda italia au tuonane paradiso, hizo sio za sifa sasa najua wewe utafanya zoezi la nyimbo unazozijua ili kufahamu zina ujumbe gani na ziko katika kundi lipi kati ya hayo niliyokufundisha hapo juu.

Baadhi ya maandiko yanayo onyesha aina za kusifu na kuabudu kwa:

1. Kusimama (Zab 135:1-2, 134:1)

2. Kuinua mikono (Zab 134:2, 28:2)

3. Kuinama au kupiga magoti (Zab 95:6)

4. Kupiga makofi (Zab 7:1)

5. Kucheza (Zab 149:3, 150:4, 2Sam 6:14)

6. Kicheko (Zab 126:2, Ayu 8:20-21)

7. Kufurahi (Kumb 12:11-12, Law 23:40)

8. Kutembea (2Nya 20:21-22)

9. Shangwe (Zab 95:1)

10. Kupiga kelele (Zab 66:1, Law 9:23-24)

11. Kupiga vigelegele (Zab 33:1, 32:11)

12. Ukimya (Mhu 3:7)

13. Kupaza sauti (Isaya 12: 6, Zab 42:4)

14. Kulia/ kutoa machozi katika roho mtakatifu

Mathayo 6:33 Utafuteni kwanza ufalme wake na haki yake na hayo mengine mtazidishiwa.

Ushuhuda wa matendo makuu ya Mungu

Mr David alishuhudia Mungu alivyomtetea kazini kwake na kupandishwa cheo kuwa mkuu wa kitengo

Mr Mgita na mkewe walishuhudia Mungu alivyoweza kuwaponya kwenye ajari ya gari lao wakati wanatoka Msoma kuja Dar na familia yake gari iliumia sana lakini wao walitoka wakiwa wazima kabisa sifa kwa Bwana.

Mr emanuel Malunda yeye alishudia Mungu alivyomponya mama yao ugonjwa wa ukoma wakati wa maombi ya kumaliza mwaka jana ya siku 3 kavu.

Mr Lumezi Papaa yeye alishuhudia Mungu alivyomsaidia hata kupata ofisi yake mwenyewe maeneo ya upanga huku akiwa hana kitu mungu alimfanikisha na sasa anasonga mbele.

Watumishi wa Bwana wa majeshi katika picha Mch Kanemba na mama Mch

Mtumishi wa Bwana Lutengano katika moja za ibada TAG Magomeni.
Mr&Mrs M'bezi nao walitoa ushuhuda ambavyo Mungu amewawezesha kujenga nyumba yao na kuondokana na mambo ya kupanga.
Mathayo 6:33 Utafuteni kwanza ufalme wake na haki yake na hayo mengine mtazidishiwa.
Abby katika pozi

Mwimbaji wa njimbo za Injili Kamanyonga akiimba niacheni nilinge

Bigman Mkama akitoa Shukrani Ibada ya mwaka mpya

Wakongwe wa muziki wakiwa kazini Magomeni TAG
Mathayo 6:33 Utafuteni kwanza ufalme wake na haki yake na hayo mengine mtazidishiwa.