Jumatano, 1 Februari 2012

FAHAMU NINI MAANA KUSIFU NA KUABUDU KATIKA BIBLIA

Nini maana ya kusifu na kuabudu


KUSIFU NA KUABUDU ni maneno tofauti na yana maana tofauti
1. kusifu

MAANA --- nikuelezea wasifu au wajihi za kitu au mtu. Sasa tunaposema tunamsifu Mungu inamaanisha ni KWA KUMUINUA JUU, KUSHUKURU KUMPAZIA SAUTI,KUFANYIA SWANGWE, KUJISHUSHA CHINI YAKE KWA UNYEYEKEVU,nk Zaburi 100:4

Neno hili kusifu kwa kiebrania lilikuwa na maana ya;
Tehila, yaani kutamka neno kwa kuongeza vionjo na mbwembwe zaidi. Mfano neno haleluya unalitamka (Ha, ha leluya huuu eee) Tehila ni kuwa kama kichaa unaposifu au kuabudu kwa utukufu wa Bwana. (Nilidhani labda hapa ndipo waswahili walipopata neno taahila).

Yadaa yaani kujiachia kwa Mungu (you just surrender yourself to the Lord).
Barak yaani kusaluti mbele za Bwana. Ni kuonyesha kwamba ni yeye peke yake anayestahili heshima na utukufu. Huwezi kumpigia saluti mtu usiyemwona, hivyo ni kwa njia ya kumwabudu Mungu katika roho na kweli ndipo tunapomwona kama alivyo na utukufu wake

2. Kuabudu
Neno la Kiebrania shachah lina maana ya kuabudu, kusujudia, kuinama kwa kuonesha unyenyekevu, kuonesha heshima kubwa au kuanguka kifudifudi. Neno la Agano la Kale proskuneo halikadhalika lina maana ya kubusu mkono, au kupiga magoti na kugusa ardhi kwa paji la uso kwa unyenyekevu mkuu. Maneno mengine mawili ya kuabudu yana maana ya kutumika, kufanya ibada Takatifu na kumtolea Mungu Sadaka.

Waache Watu Wangu Waondoke, Ili Wapate Kunitumikia, Dai hili Mungu alilolirudia mara kwa mara lilipelekea Farao kuwaruhusu watu wa Mungu kutoka Misri. Tangu wakati huo, Mungu, Mungu mwenye wivu, amekuwa akipambana na watu wake akiwazuilia kuabudu miungu mingine na sanamu, na badala yake wamwabudu Mungu aliye hai na wa kweli. Kutoka 7:16
Ibada ni kumtukuza Mungu na kumfurahia daima. Mungu anawatafuta watu wa kumwabudu, na kufanya ibada ndiyo wito wetu wa kwanza (Yn4:23 Lakini saa yaja, tena ipo, ambapo wale waabuduo halisi, watamwabudu Baba katika roho na kweli. Watu wanaoabudu namna hii, ndio Baba anawatafuta. Msitari wa 24 unasema Mungu ni Roho na wote wanaomwabudu imewapasa kumwabudu katika roho na kweli.). Ibada ya kweli ni pale tunapomruhusu Roho Mtakatifu atuongoze kutoka katika roho zetu au mioyo yetu kuabudu katika roho na katika kweli na sio tumaini letu ktk miiliau akili zetu Flp 3:3.

Ibada ni tendo la thamani kubwa, ni la kipekee na linamhusu Mungu (utatu mtakatifu) ambao peke yao wanastahili. Lucifer, aliyekuwa mhusika mkuu wa ibada huko mbinguni, alitaka ibada hiyo iwe kwa ajili yake, maana yake aabudiwe yeye badala ya Mungu; na hilo ndilo lililopelekea kuanguka kwake (Isaya 14 na Ezekieli 28). Hata wakati fulani alitaka Yesu amsujudie ili eti ampe falme zote za dunia lakini Bwana alikataa Mt4:8-10.

Kwa hiyo kuabudu ni ibada na tunaposema ibada sio zile taratibu za kibinadamu tulizojipangia katika ibada zetu za siku za leo, ibada za leo tumeweka mambo mengi sana na yanatumia muda mwingi sana kuliko ile maana hasa ambayo mungu aliikusudia katika agano la kale utana ibada zilikuwa zinafaywa kwa mambo makuu 2 neno la Mungu, na Kuabudu.

Kuabudu ni sehemu ya maisha wanadamu tumeumbiwa kuabudu, watuwezi kuishi bila kuabudu hapa haijalishi unaabudu nini!!! Unaweza kuwa unaabudu Mungu wa kweli au miungu kama ambavyo ukisoma bilia utaona kuna miungu mingi inatajwa mfano Baali, Dagon ink na hata leo iko miungu mingi ambayo wanadamu wanaiabudu lakini wa kuabudiwa ni mmoja tu. Na katika biblia tunaona kuaudu kwa mara ya kwanza kulikofanywa na Ibrahimu kutoka katika kitabu cha mwanzo 12: 8 Psalms 34:1 inaonyesha tunatakiwa kumwabudu Mungu kila wakati.

Kwanini tuabudu
kuabudu ni agizo kutoka kwa Mungu kutoka 20 2-4 . Psalm 96:9, Psalm 29:2 Tunapomwabudu mungu naye Mungu hufurahiwa na sisi Zephaniah 3:17 Rom 12:1-2

Your Worship = Your View of God
jinsi unavyoabudu ndiyo mwonekano wa mungu ulivyo ndani yako, haijarishi unaabudu wapi uwe peke yako au mko wengi kama unaabudu kwa kutokumaanisha au kumaanisha itajulikana tu na hivyo ndivyo mtu anaweza kujua ni jinsi gani mtazamo wako kwa Mungu wako.

KUNA NGUVU KATIKA KUSIFU NA KUABUDU
Yoshua 6:20 Matendo 16:23-26 zinaonyesha ambavyo kwa kutumia kusifu tu Mungu alishuka na kufanya lile lililokuwa hitaji lao.

Kusifu kunamfukuza adui
Psalms 50:23. 2 Nyak 20:22. Ukiwa unasifu na kuabudu humfukuza adui mbali kutokana na ukiwa kwenye ibada Mungu hushuka maana yeye anasema anakaa katikati ya sifa hivyo palipo na Mungu shetani hawezi kuwepo lazima akae mbali.akimbie mbali kabisa maana kunakuwepo na uwepo wa bwana wa Majeshi.

Je, ni wakati gani tuabudu?
Ni niyakati zote zinafaa kumwabudu Mungu. Kwa nyakati zilizotengwa Zaburi ya 100 inatuelekeza namna ya kuanza, lakini zaidi ya yote tunapaswa kuishi maisha ya ibada bila kukoma. Kwa kila tunapopumua, kwa kila wazo, kwa neno na tendo, tunapaswa kumwabudu Mungu wetu mzuri tunayemtumikia milele na milele Zab 145:1,2

mwa 12:6- Siku zilipita na watu wakafanyia ibada kwenye Hekalu na kwenye masinagogi; lakini siku hizi miili yetu ni hekalu la Mungu 1Kor 6:19 tu hekalu la Mungu sisi ibada zinatakiwa zifanyike kila wakati na si mara moja kwa wiki kama wengine wanavyo dhani.

Je, Tunafanyaje Ibada?
Biblia inatufahamisha jinsi watu walivyotumia mioyo yao, mawazo yao, mikono yao, viganja vyao, miguu yao, na midomo yao katika uimbaji. Walipaza sauti zao kwa furaha na kusujudu, kucheza, kusifu, kubariki na kushukuru.

Maneno kama halal na haleluya kutoka katika Zaburi yana maana ya kusifu, kumwinua na kumwadhimisha Bwana. Neno Yadah lina maana ya kunyoosha mikono hewani, na neno barak lina maana ya kupiga magoti katika ibada ya kumbariki Mungu. Kuitoa miili yetu katika kumhudumia Mungu na mwanadamu ni ibada pia (Rum 12:1). Watu pia humwabudu Mungu katika sanaa zao, katika uandishi wao, katika michezo ya kuigiza, katika muziki, katika usanifu wa majengo, na hata katika utoaji wa fedha zao kwa ajili ya Injili.

Kusifu na kuabudu sio kuimba tu
Watu wengi wanajua kuwa kusifu na kuabudu ni kuimba tu hapana kuna njia nyingi za kusifu au kuabudu, unaweza kutumia sanaa nyingine kumwabudu mungu au watu wengine wakamwabudu Mungu mf maigizo, ngonjera, shaili, uchoraji, upambaji au unakshi wa vitu, kujenga .nk

Ibada Kanisani
KatIka kanisa makusanyiko yetu yanapaswa kujawa na zaburi, nyimbo, na tenzi za rohoni ambazo zinaweza kuongozwa na Roho katika lugha mpya anazotupatia Yeye. Kwahiyo mikutano mingi ya kisasa haina tofauti sana na burudani za kikristo kama kwenye kumbi za starehe. Watu huwa wanaangalia tu, lakini je, wanaabudu? Uwepo wa Mungu na Roho wake katika ibada zetu utawafanya watu wasioamini kuanguka chini na kuabudu (Kol 3:16) (1Kor 14:15,16,25,26) (Efe 5:19) (Mdo 2:4).

Ibada Ya Kweli Ina Gharama
Biblia inazungumzia habari za sadaka za kusifu. Daudi alicheza mbele za Bwana kwa nguvu zake zote, na akakataa kumtolea Mungu kafara ambayo isingemgharimu cho chote (2Sam 6:14; 24:24). Wale mamajusi wa Mashariki walitoa zawadi za gharama kubwa walipokuja kumwabudu Yesu (Mt 2:9-12), na mwanamke mmoja alimpaka Yesu kwa mafuta ya gharama kubwa, akamwosha miguu yake kwa machozi yake, na kuifuta kwa nywele zake (Lk 7:36-50). Hivyo ibada yoyote inaambatana na kutoa tena vitu vyetu vya thamani.

Tunapaswa kumsifu Mungu kwa jinsi alivyo na kwa matendo yake; lakini Mungu mwenyewe anawatafuta na anawataka wafanya ibada, na si mradi ibada tu. Kusifu kwaweza kufanywa hadharani, lakini ibada mara zote ni jambo la ndani ya moyo. Kusifu mara zote kunaweza kuonekana au kusikika, lakini kuabudu yaweza kuwa ya kimyakimya na iliyofichika. Kusifu kunaonekana, kuna kutumia nguvu, kuna misisimko na furaha; lakini ibada mara zote ni heshima na hofu katika uwepo wa Mungu.
Biblia pekee inatuonesha jinsi Mungu anavyo hitaji na kutamani kuabudiwa na yeye pekee yake ndiyo anayestahili kuabudiwa.

Kusifu na kuabudu kwa siku za leo
Katika siku za leo kuna ufinyu wa mafundisho katika kusifu na kuabudu na ndiyo maana ya kuanda somo hili ili tupanuane mawazo. Watu wengi wa leo wanadhani kusifu ni kuimba kwa nyimbo zenye midundo ya harakaharaka(zouk&sebene) na ukipunguza spidi ndo kuabudu. Hasha tunaposema kusifu inatokana na maneno yaliyopon kwenye wimbo husika kweli ni ya kusifu, kama ni maneno ya kusifu tunasema ni wimbo wa sifa haijarishi speed inayotumika na hali kadhalika nyimbo za kuabudu. Watu katika kipengele hiki huwa wanachakanya nyimbo utakuta wakati wa kusifu anaimba wimbo wa kutia moyo au wa maombi, kinachotakiwa ni kujua kuwa kila jambo lina wakati wake ziiko nyimbo za mazishi, kufariji, kutia moyo, za maombi, za kusifu , na za kuabudu nk sasa usichanganye kwenye kusifu wewe unaimba parapanda italia au tuonane paradiso, hizo sio za sifa sasa najua wewe utafanya zoezi la nyimbo unazozijua ili kufahamu zina ujumbe gani na ziko katika kundi lipi kati ya hayo niliyokufundisha hapo juu.

Baadhi ya maandiko yanayo onyesha aina za kusifu na kuabudu kwa:

1. Kusimama (Zab 135:1-2, 134:1)

2. Kuinua mikono (Zab 134:2, 28:2)

3. Kuinama au kupiga magoti (Zab 95:6)

4. Kupiga makofi (Zab 7:1)

5. Kucheza (Zab 149:3, 150:4, 2Sam 6:14)

6. Kicheko (Zab 126:2, Ayu 8:20-21)

7. Kufurahi (Kumb 12:11-12, Law 23:40)

8. Kutembea (2Nya 20:21-22)

9. Shangwe (Zab 95:1)

10. Kupiga kelele (Zab 66:1, Law 9:23-24)

11. Kupiga vigelegele (Zab 33:1, 32:11)

12. Ukimya (Mhu 3:7)

13. Kupaza sauti (Isaya 12: 6, Zab 42:4)

14. Kulia/ kutoa machozi katika roho mtakatifu

Mathayo 6:33 Utafuteni kwanza ufalme wake na haki yake na hayo mengine mtazidishiwa.

Maoni 7 :

Bila jina alisema ...

hfavfe72

jken5kvs

f54yewr4t536

jnmrpayv

cwu6yq3y

Unknown alisema ...

Mungu akubariki

Unknown alisema ...

Na nyimbo za kwaya ni zipi

BEDOLA SISTERS alisema ...

Asante mno, barikiwa

Bila jina alisema ...

Umefafanua vizuri mtumishi mungu akubariki Sana

Bila jina alisema ...

Barikiwa mno

Sibita Edward alisema ...

Am blessed