Alhamisi, 17 Mei 2012

BAADA YA NDOA ZAO KUHALALISHWA ULAYA MASHOGA WATATOA BIBLIA ZAO HIVI KARIBUNI ZINAZOHALALISHA MAOVU WANAYOYAFANYA

Biblia ya Mashoga inatarajia kuitoka hivi karibuni, makampuni ya mashoga huko marekani na Mexico yako kwenye hatua za kukamilisha biblia hizo.  huku ikiwa imepotoshwa na kuwekwa vifungu ambavyo vinakidhisha matakwa yao, habari hizo ambazo zimenikwa mtandaoni zinaonyesha hayo makampuni na juhudi wanazofanya ili kukamilisha kwa biblia hizo.
 kampuni ya kwanza
inayotengeneza biblia mojawapo imefanya hivi :-zimeonyesha hapa ile picha tuliyozoea kuiona ya Adam na Eva wakiwa bustani ya edeni wao wamechora wanaume wawili wakiwa katika bustani ya eden. Na kuna sehemu nyingi wamebadilisha majina, sehemu ya Adamu na Eva wao wameandika Adam and Steve, Samson na Delila wameweka Samantha na Delila. Biblia mpya ya mashoga itakuwa sokoni wiki chache zijazo, Venom kutoka vikundi cha uifadhi wa kikristo amechukua hatua ya kulitangaza hili kuwatahadharisha watu juu ya hili. Mambo haya yanakuja siku chache baada viongozi wakubwa wa mataifa makubwa kuruhusu ndoa za mashoga,
Picha inayoonyesha Adam na Steve na si Adamu na Eva.
Kampuni ya Pink Cross Publishing, ambayo pia ndiyo iliyo tangaza toleo la kuruani ya mashoga, ilisema ipo kwenye hatua za mwaisho za kumalizia toleo baadhi ya mambo katika biblia ya mashoga. Kwenye maeneo yaliyo andikwa Mariamu na Yusufu, wanabadilisha na kuweka Mariamu na Josephina. Pia wanafunzi wote aliokuwanao Yesu ndio watakuwa mashoga, isipo kuwa Yuda msaliti. Katika Biblia hiyo mpya wanafunzi wote(mashoga) watashiriki chakula cha usiku kwa pamoja isipo kuwa Yule msaliti yani Yuda, wakiongozwa na shetani, biblia hii mpya tayari imeshapewa jina ikijulikana kama Biblia ya Mashoga. na msishangae nao kutoa hata mkanda wa yesu wa kishoga.

Kanisa la kisabato la Westboro limeahidi kuhakikisha kampuni hiyo ya Pink Cross Publishing inafanikiwa katika zoezi hilo la uuzwaji wa biblia hizo, Wanachama wa umoja wa mashoga wameahidi nao kuipa sapoti ya kutosha kampuni hiyo, katika manunuzi ya biblia hizo.
Shirika la Companion workbook pia litakuwepo kanisa hapo siku ya ibada ya shule ya jumapili kuzindua, na toleo jipya la biblia ya mashoga ya kikatoliki, nayo itatangazwa mwishoni mwa mwaka huu.

Kampuni ya pili ni
New Mexico-based Revision Studios hii ni kampuni ya utengenezaji wa filam ila wameamua nao kutengeneza biblia ya mashoga  ambayo itapewa jina The Princess Diana Bible.  Msemaji wa watengenezaji wa biblia hiyo bwana Max Mitchell amesema kuna matoleo mengi sana ya Biblia kama 116 sasa kwanini na wao wasiwe nayo ya kwao. walishaanza kuitengeneza biblia hiyo tangu mwaka 2009 na kitabu cha mwanzo tayari kina patikana. hichi ni kifungu cha kitabu cha mwanzo wenyewe adam na eva wamewabatiza ni Aida na Eve.

"And the Lord God caused a deep sleep to fall upon Aida, and she slept: and he took one of her ribs, and closed up the flesh instead thereof; and the rib, which the Lord God had taken from woman, made he another woman, and brought her unto the first. And Aida said, 'This is now bone of my bones, and flesh of my flesh: she shall be called Woman, because she was taken out of me. Therefore shall a woman leave her mother, and shall cleave unto her wife: and they shall be one flesh.' And they were both naked, the woman and her wife, and were not ashamed."
msemaji amesema kuwa biblia hiyo itakuwa na sehemu kuu mbili nayo ni The Gay Old Testament and The Gay New Testamen yaani agano la kale la mashoga na agano jipya la mashoga.

mwezi uliopita nilitoa habari za biblia feki http://martmalecela.blogspot.com/2012/04/kuwa-makini-na-biblia-feki-zilizoingia.html kama tusipokuwa makini tunaweza kupotoshwa usiangalie jina tu kuwa ni biblia fuatilia ujue imeandikwa na nani maana nae shetani wakati mwingine anajifanya ni malaika wa nuru. tuwe makini katika hili.

unaweza kutembelea
http://www.guardian.co.uk/world/2008/dec/01/princess-diana-gay-bible
KAMA UNA MAONI YOYOTE NIANDIKIE HAPO CHINI AU TUMA UJUMBE KWENYE
 NO +255 715 033 671, +255 767 033 671 AU FACEBOOK martmalecela

Hakuna maoni: