Alhamisi, 25 Juni 2015

OMBA YESU ANASIKIA YAZINDULIWA NCHINI MAREKANI NI ALBAMU YA TANO YA PENDO NKONE.

kwa mara ya kwanza Mwanamuziki wa nyimbo za Injili kutoka nchini Tanzania,Upendo Nkonne jumapili hii ameweka wakfu na kuzindua Album yake mpya ya tano inayokwenda kwa jina la ""Omba Yesu Anasikia " toka atoe album zingine za awali, uzinduzi ambao umefanyika nchini Marekani ndani ya kanisa la All Nations BreakThrough Church (ANBC) - Gahanna Ohio. upendo Nkone ni kati ya waimbaji wachache wa Tanzania ambao kwa sasa wanaenda nje ya nchi mara kwa mara kwa miariko ya kufanya huduma za uimbaji wa nyimbo za injili. 

ikumbukwe katika albamu zake za dvd kuna nyimbo nyingine anarekodia nje ya inchi katika kubadilisha mazingila lakini pia kupata ubora wa kimataifa. cd hiyo imezinduliwa katika kanisa la kiswahili huko marekani ambalo liko chini ya mchungaji Nkone na imewekwa wakfu na mchungaji kiongozi wa kanisa hilo.

Mchungaji wa kanisa la ANBC Donnis na Nnunu Nkone wakiiweka wakfu Album yake Upendo Nkonne

Mchungaji Kiongozi na mke wake wakifuatilia tamasha hilo

KAMA UNA MAONI YOYOTE NIANDIKIE HAPO CHINI AU TUMA UJUMBE KWENYE NO 0784 477775 au Whatup 0784 477775 AU FB Martin Malecela follow me in Twetter martmalecela au tembelea page yetu na ulike martmalecela.blogspot.com

Hakuna maoni: