Jumatatu, 24 Juni 2013

MC, MTANGAZAJI SAMUEL SASALI ATANGAZA NIA, CHRIST'S BOYZ WAJUMUIKA NAE

Wengi tunamfahamu Samuel Sasali au Papa Sebene. mwenye vipawa vingi katika shamba la Bwana. siku ya jana ametangaza uchumba katika kanisa la VCC huku akisindikizwa na marafiki zake wengi kutoka katika makanisa mbalimbali. Christ's Boyz kundi alilowahi kuimbia Samuel miaka ya 2000 lilishirikiana nae vizuri. miaka hiyo kundi hilo lilokuwa na waimbaji kama Samuel Sasali, Methew Sasali, Joel Sasali, Joseph Mwakibuti, Tonny MC Lamecky Aloyce Didier, Andrew Didier, Prosper Mwakitalima, Alistotle Didier, Emanuel Heri, Mitimingi, nk. ukiacha hao waimbaji wenzake wa enzi hizo pia familia yote ya Mch Sasali ilikuwepo na ndugu jamaa na marafiki kibao. blog hii inamtakia kila raheli mwana blogger huyo katika safari yake kuelekea kwenye ndoa.




Picha mpya ya familia ya Mch Sasali

Papa naona hapa mapigo yalikuwa speed kidogo na kutafakali ya mbele wanakoenda

Samuel akiwa na baadhi ya wana Christ's Boyz Aloyce na nyuma Tonny Lameck

Akiwa amekumbatiana na baba yake

Mch kiongozi wa VCC H. Nkone akiongea jambo
Hatimae mambo yakawa hivi

Wakifanyiwa maombi



KAMA UNA MAONI YOYOTE NIANDIKIE HAPO CHINI AU TUMA UJUMBE KWENYE NO +255 715 033 671, +255 767 033 671 AU FB Martin Malecela follow me in Twetter martmalecela au tembelea page yetu na ulike martmalecela.blogspot.com

Hakuna maoni: