Jumamosi, 22 Juni 2013

MUZIKI WA INJILI USITUMIKE KWA DHANA YA BIASHARA - CHRISTINA MBILINYI


 
 

Hata hivyo,  hakusita kueleza wazi kuwa baadhi ya mazingira yanawakatisha tamaa katika huduma hiyo na kusababisha waimbaji wengine kufikia uamuzi wa kupanga bei kama ilivyo kwa waimbaji wa nyimbo za mataifa 
 
Nikitaja wimbo wa ‘Nasubiria baraka’  itakuwa rahisi kutambua mapema ninayemzungumzia katika safu hii kwani wimbo huo umeokea umesambaa  na kujulikana ndani na nje ya nchi.
Dada huyu anaitwa Christina Mbilinyi (28), aliye na kipaji cha uimbaji alichokirimiwa na Mungu. Mashabiki wa nyimbo za Injili wanaposikia wimbo huo mara nyingi husimama na kucheza kwani unakubalika na kugusa maisha ya watu.
Kwa mara ya kwanza alipoanza kusikika masikioni kwa Watanzania, wengi walidhani dada huyu ni Mkenya kutokana na mpangilio wa mashairi na ladha ya uimbaji wake.
Msanii huyo amefanikiwa kushiriki mialiko mingi kwa ndani na nje ya nchi tangu alipotoa albamu ya wimbo huo mwaka 2011, amekuwa pekee kabla ya kumpata meneja aliyenaye kwa sasa.
Habari mpya kutoka kwa Christina ni sauti yake anayoipaza kwa waimbaji wa muziki wa Injili akionya uimbaji wa nyimbo hizo kutumika zaidi kama biashara.
“Sheria ya Mungu ni ngumu sana, Neno lake linasema walioitwa ni wengi ila watenda kazi ni wachache. Wengine wanafanya huduma kutoka ndani ya mioyo yao, wengine wanatanguliza sana pesa, wako kimasilahi zaidi, hiyo haipendezi,” anasema Christina.
Anafafanua kuwa kuna tofauti kati ya kuingia makubaliano na kuchangiwa gharama za mwaliko;  “Hilo linaeleweka, siyo lahisi kumwita mwimbaji bila kumwandalia nauli au marejesho ya gharama alizotumia kufika katika eneo hilo la huduma.”
Hata hivyo,  hakusita kueleza wazi kuwa baadhi ya mazingira yanawakatisha tamaa katika huduma hiyo na kusababisha waimbaji wengine kufikia uamuzi wa kupanga bei kama ilivyo kwa waimbaji wa nyimbo za mataifa.
Christina ambaye kwa sasa anatarajia kuipua albamu yake mpya itakayojulikana kwa jina la ‘Mtazamo wako’ , ni muumini wa Kikristo anayesali na kufanya huduma katika Kanisa la Mito ya Baraka lililopo Kariakoo jijini Dar es Salaam.
Christina anajivunia mafanikio kwa kufahamika na kupata ushirikiano mzuri katika jamii pamoja na kuona watu wakipata baraka na faraja  kupitia kazi yake ya uimbaji.
 “Masuala ya mali ni ahadi tulizopewa, zipo tu zinakuja kwa wingi, maana amenibariki,”anasema Christi
KAMA UNA MAONI YOYOTE NIANDIKIE HAPO CHINI AU TUMA UJUMBE KWENYE NO +255 715 033 671, +255 767 033 671 AU FB Martin Malecela follow me in Twetter martmalecela au tembelea page yetu na ulike martmalecela.blogspot.com

Hakuna maoni: