Pichani
juu na chini ni waandishi wa habari kutoka nchi mbalimbali barani
Afrika wakipiga picha za ukumbusho nje ya nyumba ya Askofu Desmond Tutu
mwanaharakati maarufu wa kutetea Haki za Binadamu.
Pichani juu na chini ni muonekano wa nje wa makazi ya Askofu Tutu ambapo kwa sasa inaishi familia yake.
Barabara inayoelekea yalipo makazi ya Askofu Desmond Tutu.
Wenzetu
Bwana wameendelea kwelikweli kila mtaa na barabara una kibao
kinachotoa maelekezo ya mahali unapokwenda, Chezea Bongo Wewe taa zetu
barabarani kila siku zinagongwa na magari na vibao vya maelekezo ya mtaa
ndio hadithi mpya manake Hakunaga……
Hii
ni Nyumba ya mtetea haki za Binadamu maarufu Askofu Desmond Tutu wa
Afrika Kusini ambaye amewahi kushinda tuzo ya Amani mwaka 1984 kwa
kuongoza harakati za kupinga ubaguzi wa rangi bila vita .
Alithibitishwa na aliyekuwa rais wa Afrika Kusini Mzee Nelson Mandela kuwa Mwenyekiti wa Kamisheni ya Haki na Maridhiano .
Hapa pamekuwa nyumbani kwa Askofu Desmond na mama Leah Tutu tangu mwaka 1975 .
Wamesherehekea maadhimisho ya miaka 50 ya ndoa katika nyumba hii ambayo bado ni makazi yao katika jiji la Johannesburg.
Kwa kuongezea tu nyumba hii ilibuniwa na Mhandisi Jo Noero mnamo mwaka 1990.
Nyumba hii imezinduliwa Oktoba 15 mwaka 2011.
Idadi
ya watu wa Afrika Kusini ni takriban milioni 52 ambapo kati yao milioni
42 ni Weusi, milioni 5 ni weupe kwa maana ya wazungu na milioni 5 ni
mchanganyiko na waasia milioni mbili 2 ambao wengi wao ni wahindi na
Wachina.
Afrika Kusini kuna lugha zisizopungua 11.
KAMA UNA MAONI YOYOTE NIANDIKIE HAPO CHINI AU TUMA UJUMBE KWENYE NO +255 715 033 671, +255 767 033 671
AU FB Martin Malecela follow me in Twetter martmalecela au tembelea page yetu na ulike martmalecela.blogspot.com
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni