Jumanne, 2 Oktoba 2012

NABII GEORDAVIE AWA MTUMISHI WA KWANZA KUNUNUA HELKOPTA KWAAJILI YA HUDUMA


Mtumishi wa Mungu na kiongozi wa huduma ya Ngurumo ya Upako mtumishi Mhe Nabii Geordavie mwenye makazi yake jijini Arusha,amekuwa ni mtumishi wa Kwanza nchini kumiliki usafiri wa anga kwa ajili ya kufanyia huduma.Kwa mujibu wa chanzo chetu cha habari mtumishi huyo anamiliki HELKOPTA na tayari anazo documents zote za umilikaji wa usafiri huo.


Hii ndiyo Helkopta ya ya mtumishi wa Mungu Geordavie

Nabii GeorDavie kwa sasa wengine wanamuita  MAESTRO licha ya kumiliki usafiri huo wa anga pia anamiliki kituo cha redio jijini Arusha kinachojulikana kama Ngurumo Fm Radio.Mwaka huu wa 2012 umekuwa wa baraka sana kwa mtumishi huyo ambapo siku za hivi karibuni alihitimu masomo ya THEOLOJIA kutoka chuo kimoja cha nje na kutunukiwa PHD ya Theolojia.


Nabii Geordavie Maestro akiwa ndani ya Ngurumo ya Upako Redio
KAMA UNA MAONI YOYOTE NIANDIKIE HAPO CHINI AU TUMA UJUMBE KWENYE NO +255 715 033 671, +255 767 033 671 AU FB Martin Malecela follow me in Twetter martmalecela

Hakuna maoni: