Jumanne, 2 Oktoba 2012

KONGAMANO LA VIJANA WORD ALIVE SINZA USIKOSE KIJANA

Kanisa la Word Alive Sinza linaloongozwa na Askofu Deogratius Lubala lililoko Sinza Mori jijini Dar es salaam, limeandaa kongamano la kipekee la siku mbili litakalowahusisha vijana kutoka sehemu mbalimbali. Kwa mujibu wa waandaaji wa Kongamano hilo, kongamano hilo litafanyika jumamosi ijayo na jumapili (Tarehe6-7/10/2012) kuanzia saa mbili asubuhi mpaka saa kumi na moja jioni ambapo chakula kitatolewa bure.Siku ya Jumapili kuanzia saa tisa mchana Kongamano litamalizika kwa IBADA KUBWA ya kusifu na kuabudu.


Pastor Isaac Mallonga mmoja wa wanenaji katika kongamano hilo


Kongamano hilo la vijana litakuwa likifanyika kila mwaka na kwa mwaka huu limebeba ujumbe usemao “CALL TO HIGHER DIMENSION”.Vikundi mbalimbali vya uimbaji vitahudumu vikiongozwa na Word Alive Praise Team.Kwa kijana yeyote ambaye ni mkazi wa jiji la Dar es Salaam hii si ya kukosa ukizingatia waalimu watakaohudumu Mungu ameweka hazina kubwa ndani yao kwa utukufu wa wake.Lets meet Sinza Mori jumamosi na jumapili.

wafuatao ni
Waalimu watakaohudumu
1.Rose Mushi
2.Pastor Isaack Mallonga
3.Pastor Daniel Musokwa
4.Lilian Modesta Mahiga
5.Pastor Deogratius Lubala  6.Ramsey Ngwelleja    
Mwl Rose Mushi atahudumu

Pastor Daniel Musokwa mmoja wa wanenaji katika kongamano hilo
Medesta lilian Mahiga mtumishi wa Mungu na mjasiliamali naye pia atahudumu
KAMA UNA MAONI YOYOTE NIANDIKIE HAPO CHINI AU TUMA UJUMBE KWENYE NO +255 715 033 671, +255 767 033 671 AU FB Martin Malecela follow me in Twetter martmalecela

Hakuna maoni: