Jumatatu, 3 Septemba 2012

SEMINA ZA MWAKASEGE ZAHAMISHIWA JANGWANI NI KUTOKANA NA VIFUSI VILIVYOJAZWA UWANJA WA BIAFRA

Mwalimu wa Neno la Mungu wa kimatafa Mwakasege amehamishia semina zake kwenye uwanja wa Jangwani ili kupisha ujenzi unaoendelea maeneo ya Biafra yaliyosababisha uwanja kujazwa vifusi. kwa muda mrefu sasa Mwakasege alikuwa akiutumia uwanja wa Biafra kufanyia semina zake mbalimbali habari zilioifikia blog hii leo zinaonyesha semina hiyo itakayo anza tar 15/09 zitafanyika uwanja wa jangwani ratiba ya awali ilionyesha kuwa ingekuwa ni biafra hivyo wale wote wahudhuliaji wa semina hizi wanatakiwa kufahamu mabadiliko hayo ya mahali ya semina itakapofanyika.


hivi ndivyo aliyosema mwalimu Mwakasege nanukuu " Bwana Yesu Asifiwe!!Semina ya Dar es salaam itafanyika uwanja wa jangwani na sio uwanja wa biafra kama tuliandika mwanzoni. Kutakuwa na kipindi cha vijana wa chuo,sekondari na walioko nyumbani siku ya jumamosi tarahe 15/9/2012 kwa Arusha(uwanja wa reli) na 29/9/2012 kwa Dar es salaam(uwanja wa jangwani) kwanzia saa tatu asubuhi mpaka saa sita mchana. Mungu awabariki sana na tunashukuru kwa maombi yenu na tunaendelea kuwaombea.

KAMA UNA MAONI YOYOTE NIANDIKIE HAPO CHINI AU TUMA UJUMBE KWENYE NO +255 715 033 671, +255 767 033 671 AU FB Martin Malecela follow me in Twetter martmalecela

Hakuna maoni: