Alhamisi, 19 Julai 2012

UNCLE JIMMY TEMU KUFANYA COCKTAIL PARTY YA KUMSHUKURU MUNGU BLOG YAKE KUTIMIZA MWAKA IJUMAA YA TAR 20 JULY


B
logger anayefanya vizuri katika Tasnia ya Habari Za Kikristo, Uncle James Temu ambaye pia ni Mtangazaji wa Kipindi Cha Rise and Shine na Sunday Special Kutoka Praise Power FM na Mmiliki na mwendeshaji wa Blog ya
                                                www.unclejimmytemu.blogspot.com
ameandaa siku maalum ya Kumshukuru Mungu kwa Blog yake Kutimiza Mwaka mmoja Mpaka Sasa.

Uncle Jimmy ameeleza kuwa blog hiyo ambayo mwezi huu wa July imetimiza Mwaka imepiga hatua kubwa sana mpaka sasa katika upashaji wa habari ndani na nje ya Tanzania.
Blog hiyo ambayo ni maalum kwa ajili ya kupasha habari za Kikristo na injili imekuwa ikisomwa na watu mbali mbali walio ndani na nje ya Tanzania kwa kipindi cha Mwaka mzima sasa na kutoa michango yao ya mawazo kwa maendeleo ya Blog hiyo.

Mwanahabari huyo James Temu au Uncle Jimmy amesema siku ya tarehe 20 July, 2012 kuanzia saa 1 usiku mpaka saa 3 usiku ameandaa Event Ya Kumshukuru Mungu itakayofanyika katika hotel ya Tamal maeneo ya Mwenge. Katika event hiyo Kutakuwa na Wanamuziki Wa Injili wanaovuma hapa nchini wakiongozwa na Dar-es-Salaam Band, Kutakuwa na Vinywaji pamoja na Chakula kitakachopatikana katika event.
Uncle Jimmy amesema Event hiyo haitakuwa na Kiingilio sababu ni siku maalum ya Kumshukuru Mungu. Pia alitoa mwito wa Kuwakaribisha Watu wote Bureeeeeeeeeeeee kabisa Bureeeeeeeeee kuweza Kuhudhuria Cocktail Thanks Giving Ya Blog hiyo inayotimiza Mwaka.
Kumbuka ni tarehe 20 July, 2012, Saa 1-3 Usiku, Kiingilio ni Bure, Kutakuwa na Live Bands, Wanamuziki wa Injili, Wacheza Filamu Mbalimbali, Watangazaji wa Radio, Wasikilizaji wa Radio na Wewe Msomaji pia Unakaribishwa kwa ajili ya Siku ya tarehe 20 July, 2012.
 
D
on’t Plan To Miss It.!


 
Kwa Hisani Kubwa ya www.unclejimmytemu.blogspot.com

KAMA UNA MAONI YOYOTE NIANDIKIE HAPO CHINI AU TUMA UJUMBE KWENYE NO +255 715 033 671, +255 767 033 671 AU FB Martin Malecela follow me in Twetter martmalecela

Hakuna maoni: