Ijumaa, 29 Juni 2012

MMAMA ALIYEZUIWA KWENDA NA BIBLIA YAKE KAZINI, ANAYEFANYA KAZI KATIKA HOTEL YENYE KASINO ASHINDA NA ARUHUSIWA KWENDA NA BIBLIA YAKE KAZINI

Tuni Parata ambaye anafanya kazi katika hotel ya SkyCity nchini New zeland ameshinda kesi juu ya boss wake ambaye alikuwa akimzuia kuwa na biblia sehemu ya kazi, kibali hicho kimepatikana baada ya kikao na boss wake huyo.
Tuni Parata akiwa na biblia yake ndogo aliyokutwa nayo
Ms Parata akutana meneja wa mchana wa leo baada ya baada ya kuandikia barua ya kujibu kuonekana akiwa na  biblia sehemu ya kazi kitu ambacho hakiruhusiwi kwenye kasino hiyo kitendo ambacho kingeweza kumfukuzisha kazi. Katika kikao hicho imeonekana kubeba biblia siyo utovu na nidhamu na ametakiwa aendelee kubeba biblia yake ili mradi tu iko kwenye pochi yake na anaweza kuisoma wakati wa mapumuziko.
Nimefurahisha na kikao hichi na nimeruhusiwa kuendelea kuja na biblia yangu, alisema ms Parata huku akionyesha uso wa furaha.
Mkurugenzi wa Unite Union national Mike Treen nae alishangazwa na uamuzi uliokuwa umechuliwa na hoteli ya SkyCity had haukuwa na umuhimu wowote.

akifurahi baada ya kuruhusiwa kuwa nayo hapa yuko na Mchunhaji wake
Awali mama huyo alituhumiwa kwa kosa la kukutwa na biblia kwenye pochi yake ambapo walisema ni kinyume cha utaratibu wa kazi wa hoteli hiyo, wengine walisema kuwa huwa anasoma biblia yake akiwa kaunta na kusababisha hata wateja kuondoka maana wengine hawapendi kuona kitabu hicho. Pamoja na tuhuma hizo zilizokuwa zinamkabili mama huyo ambaye amekuwa mfanyakazi wa hoteli hiyo kwa miaka 16 sasa. Aliwajibu kwa kusema kuwa hawezi kuishi bila hiyo biblia maana imekuwa ni sehemu ya maisha yake. Na alikuwa tayari hoteli ichukue hakua kali ikiwapo hata kufukuzwa kazi lakini si kuachana na biblia yake.
KAMA UNA MAONI YOYOTE NIANDIKIE HAPO CHINI AU TUMA UJUMBE KWENYE NO +255 715 033 671, +255 767 033 671 AU FB Martin Malecela follow me in Twetter martmalecela

Hakuna maoni: