Ijumaa, 27 Aprili 2012

DUNIA IMEISHA MISRI KUPITISHA SHERIA YA WANAUME KUFANYA TENDO LA NDOA NA WAKE ZAO WALIOKUFA NDANI YA MASAA 6 BAADA YA KUFA


Bunge la nchi ya Misri liko njiani kupigia kura miswada miwili ya sheria 1 wanaume na wanawake kuruhusiwa kufanya tende la ndoa na wenzi wake aliyekufa ndani ya masaa 6 baada ya kufa na 2 kushusha umri wa mwanamke kuolewa hadi miaka 14. ina maana kama mswada huo ukipitishwa kuwa ni sheria itakuwa ni nchi ya kwanza dunia kuwa na utaratibu ambao unashangaza watu, wa kufanya tendo la ndoa na mwenzi wako kwa mara ya mwisho ndani ya masaa 6 baada ya kufa. Mswada huu umekuja baada ya mshemanzi  wa Moroko ndugu Zamzami Abdul Bari kusema  masuala hayo Mei 2011, kwamba ndoa bado ni  halali hata baada ya kifo na kuongeza kuwa pia mwanamke ana haki sawa ya kushiriki kufanya ngono na mume wake aliyekufa. Miaka miwili iliyopita Zamzami alichochea utata huo na zaidi alisema ni ruhusa kwa wanawake wajawazito kunywa pombe Kwenye  nchi hiyo ya  Moroko. lakini ikaonekana maoni yake hayo ni dhaifu huko Moroko na wala hayakufuatwa. lakini cha kushangaza ni kuona kuwa suala hilo limepata nguvu sana katika nchi ya Misri mwaka huu hata kutaka kulihalalisha kupitia bunge lao. Ukiachana na sheria hiyo vilevile wamepanga kushusha umri wa mwanamke mpaka miaka 14 kuruhusiwa kuolewa.

Japo nchi ya Misri ni moja ya nchi ambazo wanaruhusiwa kuoa wanawake hadi 4 imeushangaza umma kwa hatua wanayoiendea hata hivyo kiongozi wa wanawake Dr  Mervat al-Talawi (National Council for Women .NCW) nchini humo amepinga kupitishwa kwa sheria hiyo nchini kwao, habari zaidi zinasema amemwandikia barua spika wa bunge Dr. Saad al-Katatni ili kupinga sheria hizo kupitishwa bungeni maana zinamkandamiza mwanamke. Mambo hayo yanatokea kipindi kifupi tangu aliyekuwa rais wa Misri Hosni Mubarak  kuondolewa madarakani na nguvu ya umma February 2011. Katika nyakati hizi za mwisho kumekuwa na vituko vingi vinavyotokea maana kuna tukio la kufafana na hili la kijana mmoja huko Thailand kufunga harusi na maiti mapema mwaka huu soma kwa kufuata link hii http://www.martmalecela.blogspot.com/2012/04/maajabu-ya-dunia-kijana-afunga-ndoa-na.html. Lakini kwa mtini tujifunde tunapoona matawi kuchanua tujue muda umekaribia, na mwana wa Adamu atakuja kama mwivi tunatakiwa tujaze taa zetu mafuta na kumngoja bwana harusi. ubarikiwe

KAMA UNA MAONI YOYOTE NIANDIKIE HAPO CHINI AU TUMA UJUMBE KWENYE NO +255 715 033 671, +255 767 033 671 AU FACEBOOK martmalecela

Hakuna maoni: