Jumapili, 31 Mei 2015

FLORA MBASHA KUZINDUA DVD YA NIPE NGUVU YA KUSHINDA MAJARIBU



Baada ya kutokuonekana kwa muda sasa katika matamasha hatimaye Mwimbaji Flora Mbasha tar 14/06/2015 atazindua DVD yake mpya inayokwenda kwa jina la nipe nguvu ya kushida. DVD hiyo  ina nyimbo 10. Flora amesema DVD hiyo imetengenezwa chini ya studio yake inayoitwa flem record, amesema pia tamasha la kipindi hichi atalifanya kwa namna ya tofauti ambapo nyimbo zote atakazoimba zitaimbwa live na hata sasa yuko kwenye maandalizi makubwa pamoja na mazoezi ili kuwapa radha adimu wote watakaohudhulia siku hiyo. alipoulizwa kwanini ataimba live tofauti na ilivyozoeleka kutumia cd, alisema Nitaimba live maana huo ndiyo mziki wenyewe radha watu wameshasikiliza sana cd nyumbanikwake, Hivyo mtu anapokuja ategemee kupata Vitu vizuri zaidi vyenye upako zaidi. 

alipoulizwa kuwa watu hawajakuona kwenye matamasha kwa muda sasa wategemee nini kuona kutoka kwako alijibu Watu wategemee kazi nzuri na nyimbo zenye nguvu ya kubwa Mungu Kwani Lengo langu ni kumtangaza YESU kwa dunia nzima wajue na wamsifu na kumtumaini yeye peke yake. mpaka sasa mgeni rasmi katika uzinduzi huo hajajulikana ijapo alisema atajulikana muda si mrefu. swali la mwisho kwa Flora lilikuwa  nini kitafua baada ya uzinduzi wake nae alisema Baada ya kuzindua hapa Dar inategemea kwenda Mwanza na Arusha na baada ya hapo atatangaza ratiba nyingine na alimaliza kuwaomba watu kujitokeza kwa wingi kwenye tamasha lake kwani watu watamwona Mungu lakini pia watapata kununua DVD yake hiyo mpya ambayo itapatikana siku hiyo kwenye uzinduzi waimbaji wengine wataosindikiza uzinduzi huo ni pamoja na Edson Mwasabwitwe, Christopher Muhagila, Neema Gasper, Madam Ruti, Tumaini Njole pamoja na Mahanaimu bendi
 


KAMA UNA MAONI YOYOTE NIANDIKIE HAPO CHINI AU TUMA UJUMBE KWENYE NO 0784 477775 au Whatup 0784 477775 AU FB Martin Malecela follow me in Twetter martmalecela au tembelea page yetu na ulike martmalecela.blogspot.com

Hakuna maoni: