Jumatatu, 20 Oktoba 2014

UJIO WA WIMBO MPYA WA ROSE MHANDO, JIWE CHINI YA SONY MUSIC

Msanii maarufu namba moja wa Africa Mashariki wa nyimbo za injili amefyatua  kibao cha pili kingine kilichotengenezwa katika studio za Sony Music Africa, ambapo kibao cha kwanza kiliitwa Wololo kilichobeba albam ya Yesu Kung’uta chini ya usimamizi wa Rock star 4000 na kupatikana rasmi kupitia kampuni ya Mkito.com
 
Wimbo wa jiwe umetengenezwa na kuchezwa na Rose Muhando ambapo kupangiliwa na kuzalishwa na Yusuph Mayige katika Studio ya Sony Music Afrika na kuendelezwa na  kuongezewa vionjo na  Rockstar 4000.
 Displaying IMG-20141001-WA0018.jpg
" Rose Muhando asema wimbo huu unatambulisha kuwa naniataendelea kuitawala hii dunia na kila kilichomo ndani yake, katika dunia hii ya sasa , tunapoteza uaminifu nakumsahau Mungu katika kutawala kila kitu. Ni miminatakiwa kuweka muda wa kumkumbuka na kumsifuyeye kwa njia ileile tunayotumia katika kusifu nyota zetukwa majina tunayoyajua wenyewe ila mungu wetu nimkuu kuliko majina yote makuu, Mungu Mwamba, “Jiwe”.
Displaying IMG-20141001-WA0019.jpg
Rose Muhando amejulikana kuwa msanii mahiri na wa kwanza Afrika Mashariki na pia amefanikiwa kukutana na viongozi wakubwa wa serikali akiwemo Mheshimiwa Rais wa muungano wa Tanzania Dokta Jakaya Mrisho Kikwete, Rais mstafu wa Kenya mheshimiwa Daniel Arap Moi na viongozi wengi wa siasa.
Kwa takwimu ya usambazaji wa muziki Rose Mhando amekuwa msanii wa kwanza  kuongoza mauzo ya muziki wa injili Afrika mashariki.
DVD ya albamu yake inatarajiwa kufyatulia msimu wa  krismasi.


KAMA UNA MAONI YOYOTE NIANDIKIE HAPO CHINI AU TUMA UJUMBE KWENYE NO 0784 4777775 au Whatup, +255 767 033 671 AU FB Martin Malecela follow me in Twetter martmalecela au tembelea page yetu na ulike martmalecela.blogspot.com

Hakuna maoni: