Jumanne, 9 Julai 2013

HUU NI MWAKA WA CHRISTINA SHUSHO ATWAA TUZO NYINGINE YA KIMATAIFA

Kwa miaka mitatu mfurulizo amekuwa akishiriki mashindano hayo na mwaka huu kaibuka kidedea


Mwimbaji nyota wa gospel nchini mwanamama Christina Shusho ametwaa tuzo ya mwimbaji wa mwaka kwa nchi za Afrika mashariki katika tuzo za Africa Gospel Music Awards zilizofanyika usiku wa kuamkia leo jumapili katika ukumbi wa The great hall chuo kikuu cha Queen Mary jijini London nchini Uingereza.

Shusho amepata tuzo hiyo katika kinyang'anyiro cha waimbaji wapatao tisa kutoka Kenya pamoja na Uganda huku Tanzania ilikuwa ikiwakilishwa na waimbaji wawili, Shusho pamoja na Martha Mwaipaja ambapo hii ni mara ya tatu kwa Shusho kuingizwa katika kinyang'anyiro hicho na hatimaye safari hii kura zimetosha ameondoka na tuzo ambayo imepokelewa kwa niaba yake na mkurugenzi wa GK Ambwene Mwamwaja.
Pamoja na Christina Shusho mwimbaji aliewika zaidi kwakuondoka na tuzo mbili kati ya tatu alizopendekezwa ni mwanamama Ntokozo Mbambo wa Nqubeko ambaye hata hivyo hakuhudhuria tuzo hizo ambazo zilikuwa na kasoro za kiufundi za hapa na pale huku mwimbaji kutoka DRC mwenye makazi yake nchini Uingereza bibie Dena Mwana aliweza kuwasimamisha watu kwa uhodari wake katika uimbaji. Kiujumla waimbaji kutoka Afrika magharibi, Ghana na Nigeria wameondoka na tuzo hizo zaidi ukilinganisha na waimbaji kutoka sehemu nyingine.
Mwaka jana alikuwa blogger Samu amuwakilishe Shusho lakini hakupata mwaka huu kawakilishwa na blogger Ambwene big  up bloggers, pembeni ni kijana Karabo Mongatane wa Afrika ya kusini ambaye amenyakua tuzo ya album ya mwaka kwa wapigaji wa Afro Jazz.
Christina Shusho.

blog hii inampongeza sana Christina kwa mafanikio hayo, Mungu azidi kumnyanyua kutoka hatua moja kwenda  nyingine. Pia hongera sana kwa Martha Mwaipaja kwakuweza kutambulika kimataifa, kitendo cha jina tu kuwemo katika kinyang'anyiro ni hatua kubwa sana kimuziki. Kwa pamoja muendelee kumuomba Mungu awape nyimbo za kuponya na kuwarejesha watu kwa Kristo na hatimaye siku ile ya mwisho wote tuvishwe taji.
KAMA UNA MAONI YOYOTE NIANDIKIE HAPO CHINI AU TUMA UJUMBE KWENYE NO +255 715 033 671, +255 767 033 671 AU FB Martin Malecela follow me in Twetter martmalecela au tembelea page yetu na ulike martmalecela.blogspot.com

Hakuna maoni: