Jumapili, 5 Mei 2013

KONGAMANO LA VIJANA LILILOANDALIWA NA VHM LATIA FORA ZAIDI YA VIJANA 4000 WAHUDHULIA NAFASI NA VITI VYAGOMBANIWA, WAPO WALIOKUJA KUTOKA MIKOANI NA NJE YA TANZANIA

Huduma ya VHM wameweza kuwafikia vijana wengi kwenye kongamano kubwa lililofanyika katika ukumbi wa kanisa la TAG Mwenge. Kongamano hilo lililofundishwa na mwalimu P Mitimingi limeweza kukusanya vijana wengi sana hata kuvuka malengo ya idadi ambayo walitalajia kufika. nafikiri utakubaliana na mimi siku za leo kumekuwa na mwamuko mdogo wa makusanyiko hasa kwenye makongamano lakini VHM wameonyesha kuwa bado inawezekana kuwakusanya watu ili mradi wajue nini wanachoenda kukipata.

VHM ukiacha huduma nyingine wanazofanya wamekuwa na mzigo na vijana hivyo huaanda semina na makongamano kwaajili ya kuwafundisha vijana mambo ya ujana na ya kiroho, katika kongamano hilo vijana zaidi ya 4800 ambao walihudumiwa kiroho na kimwili, ninamaanisha kuwa baada ya kufundishwa walipewa chakula bure kama ambanyo makongamano yanayoandaliwa na wamarekani. lakini sasa VHM wameweza kufanya na iwe changamoto na kwa waandaaji wengi kuwa inawezekana kama wakijipanga.




 












Watu wakipiga menu ya kueleweka kama ulaya vile unakula kiroho na kimwili

Hata watoto wa mama mdogo walikuwepo hapa akiteta na mwalimu


BAADHI YA SHUHUDA KWA WALIOHUDHULIA KWENYE SEMINA


MSIKILIZE BINTI HUYU!
Shikamoo mtumishi, naitwa ....., juzi nlikuwa kwenye seminar ya vijana uliyoiandaa, na mwisho wakati wa maombezi ulisema kuna mtu amemkasirikia Mungu kwa ajili ya matatizo lakini Mungu analo neno kwamba ananipenda, ni mimi na kabla hujaongea nlikuwa nimetoa sadaka na kuinganisha na maombi ya kutaka nimsikie Mungu akisema na mimi nimsikie kwa sababu nlishawahi kuwa mwana maombi lakini nikaacha kuwa mwanamaombi kwa sababu ya matatizo na changamoto za dunia hii sasa nataka kuanza kwa upya baada ya semina hii endelea mbele mtumish....


SHUHUDA ZAMIMINIKA KUTOKA KWA VIJANA!
Mimi kijana kutoka DUCE .mim ni mkristo, .kwanini makanisa mengi hawafundishi mambo kama haya uliotufundisha? toka niko huko sikuwahi pata semina kama hii imeyabadilisha sana maisha yangu.nitafungua akaunt kwa ajili ya huduma ya vijana.mimi nimepona nao wapone! huku mikoroshin Temeke vijana wamekata tamaa sana wanaacha wokovu hadi wadada wanavuta bangi na uovu mwingi tunahitaji mafundisho zaidi...


TESTMONY FROM ONE OF A YOUTH WHO ATTENDED YOUTH CONFERENCE MAY 1ST
P Mitimingi, be blessed by our owe some God for what you did. You know healing power speeded over all youth those attended your seminar was authentic power that its positive effect will no end i'm healed from masturbation and i believe in God will grant me a wise partner. its now over am free from fornication.


 pamoja na shuhuda hizo hapo juu pia blog hii ilitaka kujua mawili matatu kutoka kwa mtumishi wa Mungu na hivi ndivyo alivyosema


  • Martin Malecela

    Mtumishi malengo ya kongamano uliloandaa limefikia malengo kwa asilimia ngapi? na je mmeweza kuwahudumia vijana wote waliofika
  • Peter Mitimingi

    Nadhani limezidi malengo tulilenga vijana 2000 wakaja vijana 4800
    Shuhuda za uponyaji ni nyingi sana kupita maelezo

  • Peter Mitimingi

    pia kulikuwa na waislamu wengi sana
    vijana 30 waliokoka siku ile pale
  • Martin Malecela

    na waliotoka nje ya ya Dar au nje ya nchi
  • Peter Mitimingi

    Tanga, Arusha moro, Pwani Iringa
    Nje ya nchi ni Malawi na Zambia
    mmoja USA
    wa Tanga walikuwa zaidi ya 10 tena hawakuwna ndugu yoyote hapa Dar ilibidi kuwalaza ofisi za vhm
  • Martin Malecela

    duuu ok hongera kwa kazi kubwa
  • Peter Mitimingi

    kweli ilikuwa kubwa twashukuru
 
KAMA UNA MAONI YOYOTE NIANDIKIE HAPO CHINI AU TUMA UJUMBE KWENYE NO +255 715 033 671, +255 767 033 671 AU FB Martin Malecela follow me in Twetter martmalecela

Hakuna maoni: