Jumamosi, 12 Januari 2013

WAINJILISTI WA KKKT WAINGIA KAZINI















Arusha Magharibi katika Dayosisi ya Kaskazini Kati ya Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), wameapa kuendeleza mapambano kwa walichokiita ufisadi wa viongozi wa Dayosisi hiyo, hadi kieleweke.  

Ili kufanikisha azma yao hiyo, wainjilisti hao zaidi ya 180 kutoka sharika 12 za Jimbo hilo wameazimia kuunda umoja ili ‘kushughulikia’ mafisadi hao katika Dayosisi yao.
Wakizungumza baada ya kukutana jana katika Usharika wa Ngateu kujadili hatma ya maandamano yao yaliyozuiwa na Polisi, wainjilisti hao ambao walidai kuwa wao ndio ‘roho’ ya Kanisa hilo, walisema hawatanyamaza wakiona waumini wao wakivurugwa na mafisadi.

“Sisi ndio roho ya Kanisa na ndio tunaotafuta waumini, hivyo kamwe hatutakaa kimya waumini wetu wanapovurugwa na baadhi ya viongozi mafisadi wa Dayosisi,” alisema Mwinjilisti mmoja huku akiungwa mkono na wenzake katika kikao hicho.

Aliongeza: “Ufisadi hasa wa mali za Kanisa ni hatua ya kuvuruga waumini wetu ambao sasa hata mahudhurio katika ibada za sharika mbalimbali yamepungua na hilo hatutalinyamazia hata kama wote tutafukuzwa. “Hata maandiko matakatifu yanasema mwanadamu akinyamaza, Mungu hatanyamaza na katika hili tuna hakika tutashinda, kwani tunasimamia Neno la Mungu,” alisisitiza huku akinukuu maneno katika Biblia.
Alisema kesho watatangaza rasmi kuundwa kwa umoja wao baada ya ibada ya Jumapili na pia hatua nyingine kali watakazochukua dhidi ya Dayosisi hiyo, baada ya maandamano waliyopanga kufanya jana kuzuiwa na Polisi.

Polisi walizuia maandamano hayo ya amani yaliyokuwa na nia ya kutaka kurejeshwa kwa Mchungaji Kiongozi wa Usharika wa Ngateu, Philemon Mollel na pia kumlazimisha Katibu Mkuu wa Dayosisi hiyo, Israel ole Karyongi awajibike kutokana na mgogoro unaoendelea ndani ya Kanisa.

Mchungaji Mollel alisimamishwa kutoa huduma za kiroho na kisha kufukuzwa kabisa mwishoni mwa mwaka jana, kutokana na kile viongozi wa Dayosisi hiyo walichodai kuwa ni kutenda makosa yasiyovumilika.
Hata hivyo, hatua hiyo ilitokana na msimamo wa Mchungaji Mollel kusimamia kidete uwajibikaji kwa viongozi wa Dayosisi wanaotuhumiwa kuhusika katika ufujaji wa mali za Kanisa hilo katika vikao halali vya Kanisa hilo.

Mgogoro unaoendelea katika Dayosisi hiyo unatokana na madeni makubwa inayodaiwa Dayosisi kutokana na mikopo inayofikia Sh bilioni 11 zilizokopwa kwa ajili ya ujenzi wa Hoteli ya kitalii ya Arusha Corridor Springs na Hospitali ya Rufaa ya Selian zilizopo jijini hapa.

KAMA UNA MAONI YOYOTE NIANDIKIE HAPO CHINI AU TUMA UJUMBE KWENYE NO +255 715 033 671, +255 767 033 671 AU FB Martin Malecela follow me in Twetter martmalecela

Maoni 3 :

Bila jina alisema ...

I like thе valuable info уou ρrονide in
your articles. I ωill bоoκmark your weblοg anԁ checκ agaіn
here гegularly. I am quite сеrtain I'll learn a lot of new stuff right here! Good luck for the next!

my web-site; pikavippi
Review my homepage :: pikavippi

Bila jina alisema ...

Put it off! Or maybe not! I just submitted to Martin’s e-mail tackle originating from a different site this period I didnrrrt get
an mistake message. It indicates this individual probably became the knowledge this individual required
by me (account variety, etcetera) now clogged my own e-mail
correct with the mistake meaning which will states “Eric’s e-mail handle seriously isn't valid anymore”, but it’s most likely working just as before. Evidence is My spouse and i provided a message so that you can the target at a distinct spot (considered one of my personal other e-mail handles) i didn't have an problem message… darn…tghthgthgg Victor help myself adhere to my personal
continue with your corporation. I've got witout a doubt routed this application for your enterprise electronic mail, you need to I want your own pressing response.
My website :: Criminal background

Bila jina alisema ...

You should think of broadcasting press releases in your area or nationally if you have something new in relation to your website. If you, it a very good idea to syndicate your pr releases as a method of increasing your search engine optimisation method. It is possible to do and costs absolutely nothing! [url=http://www.x21w12w21.info]Vi7765ity[/url]