Alhamisi, 13 Septemba 2012

FILAMU YA MTUME MOHAMED YALETA TAFLANI KATIKA NCHI ZA KIARABU NI ZAIDI YA THE PASSION

Maandamano nje ya Ubalozi wa Marekani nchini Misri
 
Kumezuka ghasia zaidi nje ya ubalozi wa Marekani mjini Cairo kati ya polisi na waandamanaji wanaokashifu filamu ambayo wanasema kuwa inakejeli imani ya Kiislamu.
 
Runinga ya Misri ilionyesha gari likiteketezwa moto na watu wengine wakikimbia vitoza machozi.
Waandamanaji walitaka kufukuzwa kwa balozi wa Marekani nchini humo huku polisi wakiwafyatulia mabomu ya kutoa machozi waandamanaji waliokuwa wakirusha mawe.
Nchini Yemen waandamanaji wamevamia ubalozi wa Marekani wakichoma moto magari kabla ya vikosi vya ulinzi kuwadhibiti kwa kuwafukuza kutoka eneo hilo.

Maandamano zaidi pia yamefanyika katika nchi za Tunisia, Morocco, Sudan, Mauritania na Iran.
Wakati huohuo maafisa wa Marekani wanasema serikali ya nchi hiyo inachunguza ikiwa mashambulio ya jumanne kwenye ubalozi wa Marekani katika mji wa Libya wa Benghazi yalikuwa ni ya kupangwa au la .

Balozi wa Marekani nchini Libya , Christopher Stevens, aliuawa .
Maafisa wa Marekani wameelezea mashambulio hayo kama yenye utata na yenye kupangwa kitaalamu na kuna tetesi kwamba makundi ya jihad huenda yalihusika .

Awali ilifikiriwa kuwa mashambulio hayo yalikuwa na uhusiano na maandamano ya kupinga filamu iliyokuwa inamkejeli Mtume Mohammed.

Takriban waandamanaji mia mbili wamekusanyika karibu na ubalozi wa Marekani mjini Cairo Misri kwa usiku wa pili kuelezea hasira yao juu ya filamu hiyo .



Aliyekuwa balozi wa Marekani nchini Libya Christopher Stevens
 

Awali waandamanaji walirusha mawe kwenye ubalozi huo na vikosi vya usalama vikafyatua mabomu ya kutoa machozi kuwa tawanya.

Watu wenye silaha waliokuwa na maguruneti walichomo moto jengo la ubalozi na walioshuhudia wanasema watu hao walizingira eneo hilo.

Rais Obama amelaani vikali shambulio hilo na ameahidi kushirikiana na serikali ya Libya kuwafikisha mbele ya sheria wahusika

ANGALIA BAADHI YA SEHEMU YA PICHA HIYO
 

KAMA UNA MAONI YOYOTE NIANDIKIE HAPO CHINI AU TUMA UJUMBE KWENYE NO +255 715 033 671, +255 767 033 671 AU FB Martin Malecela follow me in Twetter martmalecela

Maoni 1 :

martin alisema ...

ndugu zetu waislam wamekosa uvumilivu hasa kumuua balozi wa usa libya kwa inshu ya hiyo video wakidhani wanamtetea Mungu, kumbe hakuna mwanadam awezaye kumtetea ila yeye mwenyewe! kwani! wale wote wanaofanya dhambi Mungu anashindwa kuwazuia? hasha anao uwezo wote! sasa, kama wameona kuwa kwa kutoa video hiyo ni kumkashif mtume wa Mungu kwa nn wacmuachie Mungu ahukumu?