Jumatatu, 11 Juni 2012

MAKOMA KUTUMBWIZA KENYE TAMASHA LA UTOAJI WA TUZO ZA AFRICA GOSPEL MUSIC AWARDS 2012

Zikiwa zimebaki kama siku 25 hivi kufikia siku ya utoaji wa tuzo za Africa gospel music award, watu watakao imba kwenye tamasha hilo wataja. tamasha hilo litakalofanyika tar  7/7/2012 siku ya jmosi nchini uingeleza, kati ya vikundi vingi vitakavyoimba siku hiyo ni pamoja na kundi la Makoma ambao ni wakongwe katika uimbaji wa nyimbo za injili na emmy Kosgei kutoka Kenya na waimbaji mbali mbali kutoka katika nchi nyingine za Africa. Tanzania haina mtu aliyealikwa kwenda kuimba ila tunawakilishwa na mwimbaji pekee Christina Shusho kwa miaka miwili mfululizo sasa kugombea nafasi za kupewa tuzo. hata hivyo watanzania tunatakiwa kumsupport shusho kwa kumpigia kura nyingi ili aweze kunyakuwa taji anazogombea ambazo ni mwimbaji bora wa kike afrika na afrika mashariki unaweza kutembelea http://www.africagospelawards.com/ kwaajili ya kupiga kura.
Kundi la Makoma


Christina Shusho Mshiriki pekee kutoka Tanzania
waimbaji wengine watakao imba angalia tangazo hapo chini.

KAMA UNA MAONI YOYOTE NIANDIKIE HAPO CHINI AU TUMA UJUMBE KWENYE NO +255 715 033 671, +255 767 033 671 AU FACEBOOK Martin Malecela follow me in Twetter martmalecela

Hakuna maoni: