Jumapili, 10 Juni 2012

BLOGGERS NA WANDISHI WA HABARI WAVAMIA TAMASHA LA JOHN SHABANI

Leo kuanzia saa 8 za mchana kulikuwa na tamasha la kumwabudu Mungu na kuliombea taifa la Tanzania lililoandaliwa na mwalimu John Shabani tukio hilo lilienda sambamba na uzinduzi wa DVD na BLOG yake katika hali isiyokuwa ya kawaida ukumbi ulivamiwana waandishi wa habari ili kuweza kuandika matukio katika vyombo vya habari, TBC 1 na Mlimani TV walikuwepo, na Bloggers wa kumwaga kama kawaida nimependa support kubwa waliyotoa kwa mwanabloger mwezao aliyekuwa anazingua hiyo Blog yake. kama kawaida bloggers wakifika sehemu utawajua kila mtu na kibegi cha laptop kama wanafunzi na digital camera na mara moja wakifika sehemu ya tukio si waoga hata kidogo wanapita huku na huko ili kuhakikisha wanapata habari sahihi. waliokuwepo ni Papaa. Uncle Jimmy, Victor, Rulea, Martin malecela, Tunu, na bloger mtarajiwa Faraja Mdeme.  Blog hiyo ya John Shabani  iliyotengenezwa na Rulea imezinduliwa na Waziri wa habari vijana utamaduni na michezo Mhe DR Fenella Mkandala
Baadhi ya Bloggers wakiwa busy na laptop zao kuhakikisha habari zinawafikia wahusika wa kwanza ni Victor, Papaa, Tunu wengine hawako pichani
Pamoja na kuchukua Habari pia waliweza kucheza na kushududia tamasha hilo zuri. big up sana Blogger kwa support ushikiano huo utatufikisha mbali.
John Shani akiagana na mh Waziri wakati anaondoka

Waziri aliyezindua Blog ya Shabani


blog iliyozinduliwa ni http://www.johnshabani.blogspot.com unaweza kuitembelea


KAMA UNA MAONI YOYOTE NIANDIKIE HAPO CHINI AU TUMA UJUMBE KWENYE NO +255 715 033 671, +255 767 033 671 AU FACEBOOK Martin Malecela follow me in Twetter martmalecela

Hakuna maoni: