Ijumaa, 23 Desemba 2011

WANAHITAJI MSAADA WA HALI NA MALI KWA KUPATWA NA MAFURIKO


Shalom


washirika wote wa magomeni TAG tunaombwa kuwasaidia wezetu wapatao 40 waliokubwa na mafuriko yaliotokea mkoani Dar. ombi hili limetolewa na Mch kiongozi D. kanemba na kusisitiza kuwa siku ya c- max kila mtu aje kanisani na kile alicho na uwezo nacho ili kuwasaidia wenzetu waliathirika na mafuriko. Mahitaji hayo ni kama ifuatavyo, chakula mf mchele, unga, sukari,majani ya chai, chumvi,maharagwe,mafuta ya mboga,viazi nk na vitu vingine ni kama nguo, maji, sabuni, vyombo ya ndani, au hela taslimu. kuna watu wapatao ishirini mpaka sasa ni homeless wengine wamehifadhiwa kwa majirani wengine wako kwenye nyumba za kulala wageni, na wengine kama 15 hivi wako kanisani wao na baadhi ya vitu vichache walivyookoa na hawana chakula wala vitu vingine vilivyo tajwa hapo juu shime tuungane kwa pamoja ili tuwasaidie wenzetu maana sisi ni mwili mmoja na tunatakiwa kuchukuliana nao katika kipindi hiki kigumu. tunachomshukuru Mungu kwa kweli amekuwa mwema hakuna hata mshirika mmoja aliyepoteza maisha. hapa chini ni baadhi ya familia zilizokubwa na mafuriko.

1.Michael Mwaituka Mzima wao walitoka kama walivyo vitu vyote vilizama kenye maji na ukuta wa nyumba yao umebomoka

2.Mzee mwakyusa na hii imemsababishia fresha kupanda na sasa amelazwa Mhimbili

3.Mch Mshama

4.Mch Linde

5.Mama Patrick

6.Mrs Hilda Charles

7.Shemasi Joseph Madeje

8.Shemasi Kobelo

9.Familia ya Makaranga

10.Dada Mage mwalimu wa watoto

11.Grace Shirima

12.Mr Chitadu

13.Mrs Selina Jackson Muuza chapati

14.Mume wa Zena

15.Mzee Chemponda

Na wengine wengi ambao majina yao hayajaweza kupatikana mara moja kama unataka kutuma pesa tuma kwa mpesa 0767 033 671 begin_of_the_skype_highlighting 0767 033 671 end_of_the_skype_highlighting



Mungu akubariki kwa kuitikaia wito huu wa mchungaji kiongozi D Kanemba kwaajiri ya kuwasadia wenzetu--

Martin S. Malecela


Gari likiwa limetumbukia katika daraja lillilobomoka

Jeshi la wananchi wakiwa kazini kuokoa waathirika

Nyumba zikiwa zimezama eneo la Jangwani

Mafuriko eneo la Jangwani

na habari nilizoziona kupitia gazeti la mwananchi inasadikika watu 30 wamepoteza maisha kuanzia mafuriko yaanze
Mathayo 6:33 Utafuteni kwanza ufalme wake na haki yake na hayo mengine mtazidishiwa

.http://www.youtube.com/watch?feature=player_embedded&v=r9oGyGgQ-pY

Hakuna maoni: