Jumapili, 24 Julai 2011

Mkutano unaomalizika leo Tabora na matukio katika picha

Shalom,




Tunamshukuru sana Mungu kwa jinsi ambavyo anaendelea kuonekana katika mkutano wetu ambapo watu wanaponywa na kuokolewa. Wachawi wamekutana na nguvu za Mungu na watu waliolishwa sumu wamekutana na nguvu za Mungu za uponyaji.
Idadi ya wanao-okoka pia imeenda ikikua kila siku na kesho j2 tunatumai kuwa na umati mkubwa wa watu katika mkutano huu.






Wamama nao hawajabaki nyuma wako kumpokea Bwana Yesu awe Bwana wa maisha yao

Watoto nao wako mstari wa mbele kuona kila kinachopendelea.

Watoto wamejipanga ili kuiongozwa sara ya toba.


Mikono juu kumpokea Bwana Yesu.

mmojawapo ya wahubiri wa mkutano Mwinj Kazimoto akiweka mikono juu ya wenye matatizo. 

Wamemakinika kufuatilia kila kinachoendelea katika mkutano.

Hata wabibi nao hawakuwa nyuma na hawajachelewa kumpokea Yesu wakiongozwa sala ya toba.

Timu ya uinjilisti kutoka Dar wakipata kifungua kinywa cha nguvu ili wawe na nguvu za
kuhudumia mkutano aliyesimama ni Mrs E. Kipwate ambaye aliona akikaa atachelewa, Mrs Mbezi, Saimoni Bigae na Mtumishi wa Bwana Ayubu.

Timu ya wana Magomeni wakipata kifungua kinywa kwa furaha za ushindi katika jina la Yesu.

Hakuna maoni: