Alhamisi, 5 Mei 2011

Maoni ya Wasomaji

Asante kwa mambo mengi ambayo tunayapata kupitia profile yako, kwa kweli yanatupa uelewa mkubwa sana wa kuelewa ni wapi

tulipotoka, tupo na wapi tunakokwenda. maombi kwa mwamini ni lazima na ndiyo mawasiliano yetu na Mungu aliyetuumba na pasipo maombi hatuwezi lolote.


Ila yatupasa pia tutambue Mungu anasema nini au anataka tufanye nini Watanzania kwa yale tunayoomba kila siku kwa ajili ya
nchi yetu au jibu la Mungu kwa Tanzania ni lipi maana tunaoomba na tunaendelea kuomba. Mambo mengine yatupasa kuyajua, hatuwezi kuomba kwa kupiga magoti wakati wa kukemea pepo
vile vile huwezi kufunga gori bila kuwepo uwanjani na pia hatuwezi kushinda vita vya aina yeyote bila kuwa vitani. viwe vya kiroho au vya kimwili, kila mtu ana opportunity ya kufanya jambo lolote ktk mapenzi ya Mungu na likaleta mafanikio katika Kanisa na Taifa kwa ujumla. maana yote yaliyo wazi ni yetu. yaliyo sirini ni ya Mungu.


mbarikiwe sana.


siku njema.
Irene Kipwate

Hakuna maoni: