Ijumaa, 14 Novemba 2014

UTATA WAFUNIKA KIFO CHA NABII ELIYA. ALIKUWA NI MWANZILISHI WA KANISA LA SILOAM, SHIKA NENO TENDA NENO

Kuanzia jana kumekuwa na post kutoka kwa watu tofauti tofauti katika mitandao ya kijamii kutokana na kifo cha aliyekuwa mwanzilishi wa kanisa la siloam nabii Eliya. moja ya post ni hapo chini.

Kuna habari zinaenea kwa kasi katika mitando ya kijamii ya kwamba
,mwenye mafundisho tata ,Ndungu Munuo,aka Adamu wa Pili, Nabii Eliya, Bwana wa Majeshi, Mjumbe wa Mapenzi ya Mungu wa Kizazi cha Nne, Amefariki Dunia jana usiku,
Mpaka sasa hakuna tangazo rasmi la Kanisa la Siloam.


Sitofahamu hiyo inatokana na kutokuwa na taarifa za uwazi za kifo chake. kutokana na sintofahamu hiyo blog hii ilifanya mawasiliano na mmoja wa washirika wake kutaka kujua uharisia wa jambo hilo Kwa mujibu ya Mshirika niliyeongea nae amesema kuwa nabii Elia amelala na wala hajafa na hakuna kulia maana aliwaaga watu wote wakiwamo ndugu zake na familia yote na jambo hili lilikuwa linajulikana kuwa atalala na alishatafuta hadi mrithi wake ambaye ataendeleza kazi. anategemewa kulazwa mlima wa moto (nyumbani kwake) mbezi bichi siku ya tano ya umbaji ambayo ni j2. aliongeza kusema kuwa muda wa yeye kutumika wa miaka 3 ulishaisha hivyo alishamaliza kazi. alinipa mifano kuwa manabii wengi walifanya kazi kwa miaka 3 na wakawa wamemaliza kazi yao hivyo na nabii Elia kuanzia ameanza kazi miaka 3 ilishafika ni lazima aondoke ili wengine waendelee.

Mshirika huyo alikuwa anaongea kwa ujasiri na kujiamini kana kwamba alishafundishwa namna ya kujibu, kutokana na mahojiano niliyofanya nae ni kweli Nabii Eliya kafariki na maandalizi ya kumlaza nyumbani kwake zinaendelea haijafahamika kama alikuwa anaumwa au alifariki ghafla.

Aliyekuwa Nabii Eliya wa kanisa la siloam shika neno trnda neno

Nabii Eliya akiwa madhabahuni

Wafuasi wakijipanga wakati wa yeye kuingia

Kwa heri nabii Eliya


KAMA UNA MAONI YOYOTE NIANDIKIE HAPO CHINI AU TUMA UJUMBE KWENYE NO 0784 4777775 au Whatup, +255 767 033 671 AU FB Martin Malecela follow me in Twetter martmalecela au tembelea page yetu na ulike martmalecela.blogspot.com

Hakuna maoni: