Alhamisi, 9 Mei 2013

PAPA AAGIZA UCHUNGUZI WA HARAKA UFANYWE MLIPUKO WA BOMU ARUSHA

   Askofu Francisco Montecillo Padilla,(kushoto) akisalimana na Makamu wa Raisi Dkt Mohamed Gharib Bilal hivi karibuni jijini Arusha

Dar es Salaam,Tanzania
OFISI ya Kiongozi wa Kanisa Katoliki Duniani Papa Francis Jorge Mario imepokea taarifa za Kanisa Katoliki Parokia ya Ollasiti kulipuliwa na bomu nchini Tanznaia na kuiagiza serikali kutoa taarifa za uchunguzi wa suala hilo haraka

Taarifa zilizonaswa  kutoka vyanzo vya kuaminika ndani ya kanisa hilo jijini Dar es Salaam zinadai kwamba Papa Mario ameagiza serikali kutoa taarifa za uchunguzi wa suala hilo haraka.
Papa Mario amepokea taarifa hizo ambazo zilitangazwa na Rais Jakaya Kikwete kwamba ni tukio la kigaidi, huku watu watatu wakiuawa na wengine zaidi ya 70 kujeruhiwa katika tukio hilo.

Akizungumza na Redio Vatican pamoja na mitandao ya kijamii inayomilikiwa na Kanisa hilo kubwa Duniani, mwakilishi wa Papa huyo Francisco Montecillo Padilla alisema kwamba tukio hilo halikutarajiwa kabisa kwa sababu muda wote kulikuwa na hali ya utulivu na amani kanisani hapo.

"Nilipata mshtuko baada ya kusikia mlipuko wa bomu hilo, na sekunde chache nikaona majeruhi wengi wamelala chini, nikapatwa na wasi wasi huku nikiwaonea huruma majeruhi wasiokuwa na hatia lakini Askari Polisi waliwahi kunichukuwa na kunipeleka sehemu iliyotulia kwa usalama zaidi"alisema Askofu Montecillo Padilla.

Hata hivyo taarifa zaidi zinasema kwamba Ofisi ya Papa Francis tayari imeiagiza Serikali ya Tanzania kuhakikisha inakamilisha uchunguzi wa suala hilo haraka, huku pia ikionyesha nia ya kutoa msaada zaidi kwa serikali katika uchunguzi wake. Hata hivyo Ofisi ya Kiongozi huyo tayari imesha agiza Kikosi cha upelelezi cha kimataifa kutoka nchini Marekani FBI kuja nchini kuongeza nguvu katika upelelezi wa tukio hilo,tukio la aina hiyo halikuwahi kutokea nchini Tanzania, ila liliwahi kutokea katika nchi jirani ya Kenya.

KAMA UNA MAONI YOYOTE NIANDIKIE HAPO CHINI AU TUMA UJUMBE KWENYE NO +255 715 033 671, +255 767 033 671 AU FB Martin Malecela follow me in Twetter martmalecela

Hakuna maoni: