Jumamosi, 15 Septemba 2012

MAANDAMANO YA KUPINGA MKANDA ULIDHALILISHA UISLAMU YAFIKA SUDAN

 

Waandamanaji Sudan

Waandamanaji walioghadhabishwa na filamu inayodhihaki dini ya kiisilamu wameshambulia balozi za Uingereza na Ujerumani mjini Khartoum, Sudan.
 
Waandamanaji walianza kuwasha moto na kisha kuichanachana bendera ya Ujerumani na kuweka bango lenye maandiko ya kiisilamu ambapo bendera hiyo ilikuwa.
Maandamanao yangali yanaendelea katika nchi za Mashariki ya kati na Kaskazini mwa Afrika kuilaani filamu ya Marekani inayokejeli Mtume Muhammad.

Mjini Cairo, polisi waliwarushia gesi ya kutoa machozi na kuwatawanya waandamanaji takriban 500,kutoka katika ubalozi wa Marekani.
Maandamano pia yalifanyika katika mji mkuu wa Yemen, Sanaa.

Msemaji wa ubalozi wa Uingereza amethibitisha BBC kuwa maandamano yanafanyika nje ya ubalozi wa Uingereza na kusema kuwa polisi wa Sudan wako katika eneo hilo kudhibiti hali.

Hata hivyo, msemaji huyo hangeweza kuthibitisha ikiwa waandamanaji waliingia katika ubalozi huo au ikiwa maandanamo yana uhusiano wowote na filamu hiyo inayopingwa na waisilamu kote duniani.
 
KAMA UNA MAONI YOYOTE NIANDIKIE HAPO CHINI AU TUMA UJUMBE KWENYE NO +255 715 033 671, +255 767 033 671 AU FB Martin Malecela follow me in Twetter martmalecela

Hakuna maoni: