Jumatatu, 20 Agosti 2012

MFAHAMU MWINJILISTI SARAH MVUNGI

Sarah Mvungi si jina geni katika Tanzania hii haswa wale ambao mlikuwa ni wapenzi wa kuangalia michezo ya tv ya kikundi cha Kaole miaka ya 2000+. Mimi nilimfahamu kwa jina la honey na ndiyo nililolizoea, ukiachana na kuigiza mdada huyu Mungu kampa kipaji kingine cha kuimba na pia kazi yake hasa anayofanya kila siku ni muuguzi. Blog hii ilifanya nae mahojiano na ilikuwa hivi
Martmalecela: Jina lako kamili
SARAH MVUNGI: SARAH MVUNGI
Martmalecela: Unafanya Huduma gani
SARAH MVUNGI: UIMBAJI WA NYIMBO ZA INJILI,UIGIZAJI NA PIA NI MUUGUZI
Martmalecela: Ulianza lini huduma yako
SARAH MVUNGI: MITANO AU SITA HIVI.
Martmalecela: Kitu gani kilichokufanya kuvutiwa kufanya huduma hii
SARAH MVUNGI: NINAWEZA KUSEMA NI MUNGU TU KWANI NILIKUWA NAPENDa kuimba mda mrefu na nilivutiwa na waimbaji wengi wa nyimbo za ijnili wa zamani kama BAHATI BUKUKU NA JENIFA MGENDI nk
Martmalecela: Ni muimbaji gani ambaye alikuvutia hadi wewe kushawishika kuanza kuimba au hukushawishiwa
SARAH MVUNGI: BAHATI BUKUKU NA JENIFA MGENDI NA WENGINE
Martmalecela: Kwa muda gani sasa umekuwa ukifanya huduma hii
SARAH MVUNGI: MIAKA ZAIDI YA MITANO
Martmalecela: Kuna mtu yeyote aliyekusaidia wewe kufikia hapa ulipo
SARAH MVUNGI:  NI MUNGU PEKEE NDO ALINISAIDIA NATUNGA MWENYEWE NA IMBA MWENYEWE.
Martmalecela: Umeshatoa matoleo mangapi audi
SARAH MVUNGI:  NI MOJA SASA INAITWA NIACHENI NIMFUATE YESU AMBAYO IKO MADUKANI
Martmalecela: Kuna changamoto gani ambazo unakutana katika huduma yako
SARAH MVUNGI:  NI NYINGI LAKINI MOJA KUU NIPALE NINAPOONA NASHINDWA KUFIKA SEHEMU FLANI KWA SABABU NIMEKOSA NAULI I MEAN INANIUMA MAANA NAONA NAELEWEKA VIBAYA NA PIA NAKOSA KUHDUMIA WATU HASA PALE UNAPOALIKWA NA ANAEKUALIKA HAJAKUTUMIA NAULI ANAWEZA KUKUONA KAMA UNARINGA KUMBE UMEKOSA TU NAULI


 Martmalecela: Msaada gani unaohitaji kama akitokea mtu kutaka kukusaidia
SARAH MVUNGI:  MIMI NINAWEZA KUSEMA MSAADA WANGU NI GARI NA VYOMBO VYA MZIKI ILI NIWEZE KWENDA SEHEMU NA IKIWEZEKNA NIHUBIRI NIKIWA NA VYOMBO VYANGU
Martmalecela: Nyimbo zako unatunga mwenyewe au unatungiwa
SARAH MVUNGI:  NATUNGA MWENYEWE NA KUIMBA PIA HUWA NASAIDIWA NA WATU KATIKA KUIMBA CHURUS TU.
Martmalecela: Kuna mwimbaji yeyete maarufu ambaye umewahi kushirikiana nae, mtaje
SARAH MVUNGI:  NDIO NIMEWAHI KUSHIRIKIANA NA ENOCK JONAS KWANGU NI MAARUUFU KWA SABABU YUKO JUU KWA SASA.
Martmalecela: Una ushauri gani kwa wanaotaka kufanya kama wewe
SARAH MVUNGI: MUNGU NDIO KILA KITU WAMWEKE MBELE NA PIA SIO KILA USHAURI NI MZURI WAWE MAKINI NA WATU NA PIA WAWE WANAAMINI KUWA YOTE WANAWEZA.

       
KAMA UNA MAONI YOYOTE NIANDIKIE HAPO CHINI AU TUMA UJUMBE KWENYE NO +255 715 033 671, +255 767 033 671 AU FB Martin Malecela follow me in Twetter martmalecela

Hakuna maoni: