Jumatano, 12 Oktoba 2016

Je! WEWE ni SUMAKU ya MUNGU?




This is automatic! Ukianza ku-focus kwa Mungu na kuondoa moyo wako kwenye mambo yote yanayomchukiza Mungu, Mungu naye anaanza ku-focus kwako na KUJA karibu yako. Wewe unakuwa kivutio kwa Mungu kama sumaku. Hapo ni bila kuomba chochote wala kumwita Mungu; Atakuja tu.
 
Kwa maana macho ya BWANA hukimbia-kimbia duniani mwote, ili ajionyeshe mwenye nguvu kwa ajili ya hao, waliokamilika moyo kuelekea kwake” (2 Nyakati 16:9).
 
Na, ukiondoa focus kwa Mungu, na kuhamishia MOYO wako kwa mtu au miungu mjngine; Mungu anaondoka bila kufukuzwa, tena bila kuaga! Hii ndio maana halisi ya wivu; Mungu ni mwenye wivu!
 
BWANA asema hivi, Amelaaniwa mtu yule amtegemeaye mwanadamu, Amfanyaye mwanadamu kuwa kinga yake Na moyoni mwake amemwacha BWANA” (Yeremiah 17:5).
 
Kumbuka KANUNI hii, “Mkaribieni Mungu, naye atawakaribia ninyi. Itakaseni mikono yenu, enyi wenye dhambi, na kuisafisha mioyo yenu, enyi wenye nia mbili” (Yakobo 4:8) - WEWE ndio unaanza KUMKARIBIA Mungu ili YEYE akukaribie wewe; Unafanya hivyo kwa KUULEKEZA moyo wako kwake na kufanya mapenzi yake. Hapo UTANASA yale macho ya Mungu yanayo kimbia-kimbia duniani mwote kusaka watu wa namna hii.
 
Chagua leo, unataka UKARIBU na Mungu au na MTU (miungu mingine)? Kisha chukua hatua.

Frank P. Seth
 
KAMA UNA MAONI YOYOTE NIANDIKIE HAPO CHINI AU TUMA UJUMBE KWENYE NO 0784 477775 au Whatup 0784 477775 AU FB Martin Malecela follow me in Twetter martmalecela au tembelea page yetu na ulike martmalecela.blogspot.com

Hakuna maoni: