Jumapili, 28 Februari 2016

COUNSELING TRAINING - MWENGE! WATOTO WANAZALIWA WAKIWA NA DHAMBI DHAMBI YA ASILI KWA WATOTO!


1. Ukimuwekea mtoto Mungu na Shetani halafu ukampa uhuru wa kuchagua amfuate nani, wengi tunadhani kwamba mtoto atamchagua Mungu lakini ukweli ni kwamba mtoto atachagua kumfuata shetani badala ya Mungu.

2. Watoto hawawezi kuchagua kwa hiari yao kutenda mema kwasababu ya ile nguvu ya dhambi ya asili itendayo kazi ndani ya mwanadamu..
3. Ni jukumu la wazazi kuhakikisha wanaweka mkakati wa makusudi kwa mtoto/watoto tokea wanapokuwa tumboni, kabla ya kuzaliwa kuzaliwa kwao mpaka makuzi yao mpaka watakapokuja kuwa watu wazima.

4. Ni wakati gani wa kuanza kuzungumza na mtoto wako? Jibu ni kwamba ni wakati akiwa mimba. Mtoto anauwezo wa kusikia tokea akiwa mimba hata kabla hajazaliwa.
5. Wazazi wasiwatarajie watoto kuwa wema wao wenyewe bila kuhakikisha wanawawekea njia madhubuti za kimungu na kuwasisitiza watoto wao kuzifuata na kuzikataa njia za shetani.
6. Watoto wetu wameuzwa kwa shetani ili kuwarudisha lazima kuwafundisha njia za kimungu na kuwawekea mikakati ya kumjua Mungu na kumfuata vinginevyo watamezwa na dunia na kamwe Mungu hawatamtaka.
Warumi 7:14 - 20

14 Kwa maana twajua ya kuwa torati asili yake ni ya rohoni; bali mimi ni mtu wa mwilini, nimeuzwa chini ya dhambi. 15 Maana sijui nifanyalo, kwa sababu lile nilipendalo, silitendi; bali lile nilichukialo ndilo ninalolitenda. 16 Lakini kama nikilitenda lile nisilolipenda, naikiri ile sheria ya kuwa ni njema.17 Basi sasa si mimi nafsi yangu ninayetenda hilo, bali ni ile dhambi ikaayo ndani yangu 18 Kwa maana najua ya kuwa ndani yangu, yaani, ndani ya mwili wangu, halikai neno jema; kwa kuwa kutaka nataka, bali kutenda lililo jema sipati. 19 Kwa maana lile jema nilipendalo, silitendi; bali lile baya nisilolipenda ndilo nilitendalo. 20 Basi kama lile nisilolipenda ndilo nilitendalo, si mimi nafsi yangu nilitendaye, bali ni ile dhambi ikaayo ndani yangu

KAMA UNA MAONI YOYOTE NIANDIKIE HAPO CHINI AU TUMA UJUMBE KWENYE NO 0784 477775 au Whatup 0784 477775 AU FB Martin Malecela follow me in Twetter martmalecela au tembelea page yetu na ulike martmalecela.blogspot.com

Hakuna maoni: